TWITE CHINI YA UANGALIZI WA DOKTA

 
BEKI wa Yanga raia wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), Mbuyu Twite yupo chini ya uangalizi wa daktari bingwa, Gilbert Kigady wa Hospitali ya Trana Senta iliyopo Masaki, Dar es Salaam.Mchezaji huyo yupo chini ya uangalizi kutokana na uvimbe aliokuwa nao katika paja lake, baada ya kuumia wakati akiitumikia timu hiyo
. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Dar es Salaam jana daktari wa Yanga, Nasoro Matuzia alisema bado hawajajua ni lini mchezaji huyo ataanza mazoezi."Kwa sasa tunaona maendeleo yake si mabaya tangu alipoanza matibabu kwa Dkt. Kigady, ila hatuwezi kusema lini ataanza kuitumikia timu," alisema Matuzia.
Aliongeza kuwa wanafanya jitihada za kumpatia matibabu mchezaji huyo kwa kuwa wanamtegemea katika kikosi cha Yanga.

0 comments: