Usichokijua kuhusu Nash MC na maisha ya msoto aliyoyapitia hadi sasa kuitegemea sanaa, awaasa Ma-MC wasikurupuke
Nash MC ni moja kati wa wasanii ambao mara nyingi wamekuwa wakitajwa na wasanii wenzao kuwa wanaijua na kuifuata misingi ya Hip Hop, hata Madee wa Tip Top aliyewahi kusema kwenye wimbo wake ‘Hip Hop ina misingi nyie wabongo hamuiwezi’, aliwahi kutamka kwenye kipindi cha power jam kuwa mwana hip hop pekee anaemkubali Tanzania kwa kufuata misingi ni Nash MC.
Anajulikana kama Maalim Nash, na hivi sasa anataka afahamike
kama Nash MC Palestina, kupitia ukurasa wake wa Facebook alifunguka undani wa
safari yake ya muziki, misoto aliyoipitia na watu waliomsaidia hadi kufika hapa
alipo anaitegemea sanaa.
“Wakati namaliza kidato cha 4 mwaka 2003 pale benjamin
william mkapa,matokeo yalipotoka sikubahatika kufaulu wala kuendelea na elimu
ya juu,na baba yangu mzazi alikua tayari ashafariki tangu mwaka 1999,M.a.p baba
yangu,na hali za familia zetu mtaani nadhani wengi mnazijua pale unapomaliza
shule jinsi unavyochukuliwa pale nyumbani kwenu.utaanza kuambiwa uchangie hela
za mboga,unga na majukumu yanaibuka ghafla tu,nilijiuliza maswali mengi sana
hivi nitaishi vipi????
Sikua na kazi wala kibarua na sanaa haikua imestawi katika
upande wangu,kwa kweli hali ilikua ngumu sana,ila mwenyezi Mungu hakunitupa mja
wake alinikumbusha kua kuna kipaji amenipa na nachotakiwa ni kukifanyia kazi
kwa juhudi na maarifa sana,nililiona hilo na nikaanza kuzama katika utamaduni
wa hip hop kwa nguvu na akili zaidi kwa muda wa miaka mi 5 au 6 nikawa nasoma
na kujifunza mambo mengi sana juu ya hip hop kiundani mno sikukurupuka kwenda
studio na baada ya hapo nikaanza kuonekana zaidi katika matamasha ya wapi na
hatimae siku 1 nikapewa kipindi na saigon katika kituo cha eatv,na kuelezea hip
hop na misingi yake na itikadi pia watu wengi walianza kunipenda na kunikubali
sana na miaka miwili mbele nikakutana na mjomba Zavara na Lindu hawa walinipa
miongozo mikubwa sana katika safari yangu na na wimbo wa kwanza kurekodi ilikua
chini ya mtayarishaji Kita pale rama records,ulikua unaitwa, ‘nani mkali
kwenywe game’ lakini ikumbkwe kua mwaka 2000.
Niliwahi kurekodi na
gorrila killa ambao kwa ss ni pingu na deso na mwaka 2002 nilirekodi wimbo
ambao nilimshirikisha dully sykes na dogo lecha ,fm records chini ya miiika
mwamba.na wimbo huo ulinitambulisha vema kipindi kile ingawa haukua katika
misingi mizuri ya hip hop.kwa historia hii fupi napenda kumshukuru mungu na hip
hop sana kwani naweza kupata rizki kupitia hip hop! ewe mc hakikisha unasoma na
kujifunza sanaa usikurupuke kuingia studio soma mchezo kwanza!!!!!”
0 comments: