Bayern Munich kuwaacha hawa.


Bayern-Munich-Champions-League-Winners-2013-HD-Wallpaper
Mabingwa wa ulaya na bundesliga Bayern Munich wanakaribia
kuwauza wachezaji wake watatu ambao ni Diego Contento ,
Emre Can na Luis Gustavo Dias .
Wachezaji hao hawakupangwa kwenye mchezo wa jana (Jumatano)
 kati ya Bayern Munich na Sao Paolo ambapo inaaminika kuwa
 kocha Pep Guardiola amezungumza nao na kuwafahamisha kuwa
 hawako kwenye mipango yake .
Diego Contento mmoja wa wachezaji wanaotarajia kuuzwa na Bayern .
Diego Contento mmoja wa wachezaji wanaotarajia kuuzwa
 na Bayern .
Emre Can na Diego Contento wamekuwa nje ya kikosi cha
kwanza na ilidhaniwa kuwa wangeondoka Bayern msimu
 huu lakini kuondoka kwa Luis Gustavo kutawashangaza
wengi kutokana na mchango wake kwenye mafanikio ya
Bayern Msimu uliopita .
Luis Gustavo.
Luis Gustavo.
Nafasi ya Gustavo imekuwa finyu baada ya kusajiliwa kwa
 wachezaji Mario Gotze na Thiago Alcantarra ambapo anajikuta
 nje ya mipango ya kocha Pep Guardiola hali inayomfanya
alazimike kuondoka hasa katika kipindi hiki muhimu kabla ya
 michuano ya kombe la dunia inayotaraji kufanyika nyumbani
 kwao huko Brazil mwakani.
Emre Can naye atauzwa .
Emre Can naye atauzwa .

0 comments: