Yanga mwendo mdundo ikiua Azam

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik
akimkabidhi ngao ya Jamii kwa kapteni wa timu ya Yanga Nadir Haroub
`Cannavaro.`( Picha na Khalfan Said)
Ikizua hofu kwa mashabiki wake ya
kushindwa kuendelea pale ilipotwalia ubingwa wa Bara msimu uliopita,
nafasi ya Aly Mustafa ilichukuliwa na Deogratias Munishi katika dakika
ya 26 baada ya mlinda mlango huyo kuumia akijaribu kumzuia John Bocco wa
Azam asifunge.
Wakati huo, kocha wa Yanga Ernie Brandts
alikuwa ameshalazimika kumuingiza kiraka Mbuyu Twite kuchukua nafasi ya
beki Kelvin Yondani dakika 10 kabla ya kipa huyo, kutokana na sababu
hiyo hiyo dhidi ya mshambuliaji huyohuyo wa Azam.
Iliichukua Yanga inayowania pia ubingwa wa
Bara, Kombe la Kagame la Afrika Mashariki na Kati na taji la Ligi ya
Klabu Bingwa Afrika msimu huu dakika mbili tu kupata bao lililoipa Ngao
ya Jamii.
Bao hilo lilifungwa na Salum Telela kwa
shuti baada ya mabeki wa Azam kutomkaba wakidhani angeusambaza, mfungaji
akiwa alipata pasi kutoka kwa mshambuliaji wa Burundi Didier Kavumbagu.
Khamis Mcha aliipotezea Azam iliyoshika
nafasi ya pili msimu uliopita nafasi nzuri ya kusawazisha katikati ya
kipindi cha kwanza, baada ya shuti lake kuokolewa na Nadir Haroub huku
lango likiwa wazi kutokana na Mustafa kuwa alishaanguka chini langoni
mwa Yanga.
Kabla ya Mcha kupoteza nafasi hiyo,
mshambuliaji hatari wa Azam Boco alikuwa ametoka kushindwa kufunga bao
rahisi baada ya Mustafa kuokoa mpira miguuni mwake dakika nane tangu bao
la Yanga.
Kumalizika kwa pambano la Ngao ya Jamii ni
ishara kuwa pazia la msimu mpya wa ligi kuu ya Bara limefunguliwa na
sasa Yanga itakuwa mwenyeji wa timu iliyopanda tena daraja ya Ashanti
United kwenye Uwanja wa Taifa Jumamosi miongoni mwa mechi saba.
Azam itacheza ugenini Manungu Complex na
Mtibwa Sugar siku hiyo pia wakati JKT Oljoro na Coastal Union zitakuwa
kwenye Uwanja wa Sherikh Amri Abeid na Mgambo JKT na JKT Ruvu
zitapambana kwenye Uwanja wa Mkwakwani.
Timu mpya ya Rhino Rangers itaikaribisha Simba kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.
Mbeya City itacheza mechi yake ya kwanza
kabisa ya ligi kuu katika historia yake dhidi ya Kagera Sugar kwenye
Uwanja wa Sokoine na Ruvu Shooting itakuwa mwenyeji wa Prisons kwenye
Uwanja wa Mabatini mjini Mlandizi.
Timu zilikuwa:
YANGA: Aly Mustafa
(Deogratias Munishi dk.26), Juma Abdul, David Luhende, Nadir Haroub,
Kelvin Yondani (Mbuyu Twite dk.15), Athumani Iddi, Simon Msuva, Salum
Telela, Jeryson Tegete (Hussein Javu dk.67), Didier Kavumbagu, Haruna
Niyonzima.
AZAM: Aishi Manula,
Erasto Nyoni (Joakins Atudo dk.58), Nazir Salum, David Mwantika, Aggrey
Moris, Himid Mao, Kipre Tchetche, Salum Abubakar, John Bocco (Gaudence
Mwaikimba dk.74), Michael Balou (Ibrahim Mwaipopo dk.62), Khamis Mcha.
CHANZO:
NIPASHE JUMAPILI
0 comments: