0762310674-my phone no,,,,

0 comments:

j cole ft tlc-crocked smile

[Hook: TLC] I'm on my way, on my way, on my way down
I'm on my way, on my way, on my way down
You're the one that was trying to keep me way down But like the sun know you know I found my way back 'round
Learn more »

0 comments:

Hatma ya watuhumiwa wa dawa za kulevya JNIA Sept. 5



Waziri wa Uchukuzi, Dk.Harrison Mwakyembe
Hatma ya Maofisa wanne wa usalama wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) wanaodaiwa kuhusika kula njama kusafirishwa dawa za kulevya zenye thamani ya Sh. bilioni 6.8 itajulikana Septemba 5, mwaka huu.
Learn more »

0 comments:

Chadema: Tutapeleka mapendekezo yetu Katiba mpya kwa lori

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimefunga rasmi mikutano yake ya kukusanya maoni kutoka kwa wananchi kuhusu Rasimu ya Katiba mpya kupitia mabaraza huru ya chama hicho, jijini Dar es Salaam.

Chama hicho kimesema kimefanikiwa kukusanya maoni ya wananchi milioni tano na kwamba wanatarajia kupeleka maoni hayo kwenye ofisi za Tume kwa lori kwa kuwa ni mengi.

Akifunga mikutano hiyo juzi jijini humo, Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willbrod Slaa, alisema katika mikutano 49 waliyoifanya ndani ya mikoa tisa nchini, wamekusanya takribani maoni milioni tano kutoka kwa Watanzania kuhusu maboresho ya rasimu hiyo dhidi ya milioni mbili yaliyokusanywa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kutoka kwa wanachama wake.

Dk. Slaa alitoa kauli hiyo juzi katika viwanja vya Mwembeyanga wilayani Temeke, jijini Dar es Salaam, wakati akihitimisha mkutano wake wa mabaraza huru ya kukusanya maoni kwa Watanzania juu ya Rasimu ya Katiba mpya. Alisema, Chadema wanaunga mkono  Rasimu ya Tume ya  Mabadiliko ya Katiba inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba, lakini wanapingana naye katika baadhi ya vipengele kama vile Tanzania Bara kuitwa Tanganyika.


Baadhi ya wananchi waliokuwapo kwenye mkutano huo walipendekeza kuongezwa kwa vipengele vya haki kwenye tunu za taifa.

Tunu saba za taifa ambazo zimependekezwa katika rasimu hiyo ni utu, uzalendo, uadilifu, umoja, uwazi, uwajibikaji na lugha ya taifa.

Wananchi hao walipendekeza kwamba kwenye rasimu hiyo kiongezwe kipengele kinachomruhusu kila Mtanzania kuwa na haki ya kumiliki ardhi, kupata huduma bora za afya kama viongozi wa serikali na wabunge wanavyofanyiwa.

Dk. Slaa alisema katika mikutano hiyo  wamezunguka katika mikoa tisa na kufanya mikutano 49 huku zaidi ya Watanzania milioni tano wakiwa wametoa maoni yao juu ya rasimu hiyo.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Wabunge Tanzania watoka nje Bunge la Afrika Mashariki

Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kutoka Tanzania wametoka nje ya ukumbi wa Bunge ikiwa ni siku moja baada ya wenzao wa Rwanda na Uganda kufanya hivyo, wote wakipingana kuhusu utaratibu wa kufanya vikao vya bunge hilo.

Juzi wakiunga mkono hoja iliyowasilishwa na Mbunge kutoka Kenya, Peter Mathuki, wabunge wote kutoka Rwanda na baadhi wa Uganda, walitoka nje ya ukumbi wa Bunge hilo wakishinikiza hoja iliyowasilishwa na mbunge huyo kuwa vikao vingine vifanyike nje ya makao makuu Arusha ikubaliwe.

Wakati wabunge kutoka Tanzania wanapinga utaratibu unaopigiwa debe na wabunge kutoka nchi wanachama wakitaka kuwepo kwa mzunguko wa vikao vya bunge hilo, Watanzania wanataka utaratibu asilia wa EALA wa kuendesha vikao vyake makao makuu ya Jumuiya hiyo uendelee kuheshimiwa.

Wabunge kutoka Tanzania wanapinga utaratibu wa kufanya vikao kwa kuzunguka kila nchi mwanachama kwa maelezo  kuwa kufanya hivyo ni kwenda kinyume na utaratibu wa kuanzisha Bunge hilo na ni gharama kwa uendeshaji.

Katika kuonyesha hawaungi mkono utaratibu huo, wabunge kutoka Tanzania jana nao waliacha kuingia ukumbi wa Bunge ikiwa ni ishara ya kuonyesha hawakubaliani na ukiukwaji wa taratibu ya EALA.

Mbunge kutoka Tanzania, Abdullah Hussein Mwinyi,  ndiye aliyesimama na kulieleza Bunge hilo kuwa kitendo kilichofanywa na wabunge wenzao kutoka Rwanda hakikuwa cha kistaarabu.

Alisema kuwa, kitendo hicho ni dharau kwa kiti cha Spika na Bunge hilo kwani hoja iliyowasilishwa haikufuata utaratibu wa kibunge.

Alisema anasikitishwa na kilichotokea juzi bungeni hapo kwa kuwa siyo utamaduni mzuri uliozoeleka kwa bunge hilo.

“Huu ni udhalilishaji wa kiti cha Spika na kimechafua hata sifa ya Bunge lako, tunatakiwa kuweka utaratibu sawa ili kiti kiheshimiwe,” alisema. Hata hivyo, baada ya kueleza hoja hiyo wabunge wa Tanzania walitoka nje ya ukumbi huo na kusababisha kikao hicho kushindwa kuendelea, huku Mwinyi akizungumzia kitendo walichofanya wabunge kutoka Rwanda kuwa siyo cha kistaarabu.

Mbunge mwingine kutoka Tanzania, Shy-Rose Bhanji, akizungumzia tukio hilo alisema kwa mujibu wa utaratibu wa kidemokrasia hatua ambayo wameichukua ni ya kujibu mapigo kama ishara ya kupinga kitendo kilichofanywa na wenzao.

Kufuatia kutoka nje kwa wabunge hao, Spika wa EALA, Dk Margerth Zziwa, aliahirisha kikao hicho hadi leo huku akiendelea na vikao vya ndani.

Kila nchi mwanachama ina wabunge tisa ambao wanafanya idadi ya wabunge 45.
CHANZO: NIPASHE

1 comments:

picha ya siku

Shaheen Barca's photo.

1 comments:

Hii ya binti wa miaka 14 kujifungua Mapacha watatu Kenya umeisoma yote?


Kenya 
Radio station ya Kenya ‘Radio Maisha’ imeripoti kwamba wauguzi katika hospitali kuu ya Bungoma nchini humo wamepigwa na butwaa baada ya msichana mwenye umri wa miaka 14 kujifungua mapacha watatu.
Madaktari katika hospitali hiyo wanasema kuwa watoto hao wako katika hali nzuri ya afya japo mama yao bado anaonekana kuwa mnyonge.
Afisa wa baraza la kaunti ya Bungoma anayesimamia afya Grace Khayota, aliwaongoza maafisa wengine wa kaunti hadi hospitali hiyo kuwaona watoto hao ambapo sasa mama wa watoto hao Mwanarahab Wamukoya ambae ni msichana wa miaka 14, ameomba Wasamaria kumpa usaidizi kwenye kuwalea watoto.
Taarifa kwenye sentensi nyingine imesema binti huyu wa miaka 14 amepata watoto hao kutokana na uhusiano wa kimapenzi kati yake na mpenzi wake ambae ni mvulana wa miaka 16.

0 comments:

CAG aisafisha wizara ya Magufuli

Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) imeisafisha Wizara ya Ujenzi dhidi ya tuhuma za ufisadi uliohusisha Sh. bilioni 253 zilizoingia kwenye akaunti ya wizara hiyo kwa ajili ya kulipa madeni ya makandarasi na wahandisi washauri.

Tuhuma hizo dhidi ya wizara hiyo ziliibulika wakati Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali Kuu (PAC) na Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) ilipotaka kupata ufafanuzi wa matumizi ya fedha katika wizara hiyo kwa mwaka 2011/2012.


CAG, Ludovick Utouh, alisema jijini Dar es Salaam jana kuwa fedha hizo zilijumlishwa kimakosa kwenye hesabu za wizara hiyo, kama matumizi ya akaunti ya maendeleo na kuongeza matumizi.

“Kihasibu fedha hizi zilipaswa kuonyeshwa kwenye hesabu za mtumiaji halisi, ambaye ni Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads)  na siyo wizara. Hivyo, ufisadi katika hili haupo, bali ni makosa ya kihasibu,” alisema Utouh.

Kwa mujibu wa Utouh, Wizara ya Ujenzi imejenga barabara katika kona zote za nchi kwa mwaka wa fedha 2011/2012 ukilinganisha na miaka mingine.

Alisema kwa mara ya kwanza ofisi yake ilitoa kitabu cha muhtasari wa ripoti za CAG za mwaka 2011/2012 kwa lugha ya Kiswahili, ili kurahisisha usomaji na upatikanaji wa taarifa za ukaguzi wa hesabu kwa kila mwananchi.

Aliongeza kuwa Tanzania  imefanikiwa kwa mara ya kwanza kukagua hesabu za Umoja wa Mataifa (UN) na kukubalika na Bodi ya Ukaguzi ya UN.

“Fursa ya nchi yetu kukagua UN ni sifa kwa Taifa na imeweza kuitangaza Tanzania duniani, kujijengea uwezo na uelewa, kujikomboa kiuchumi, kupata kazi za ukaguzi katika mashirika makubwa pamoja na kuongeza ufanisi wa ukaguzi wa serikali na taasisi zake,” alisema.


CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Wafanyakazi 1,076 watimuliwa Tazara

Wafanyakazi 1,076 wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (Tazara) upande wa Tanzania wamefukuzwa kazi kutokana na  kufanya mgomo usio halali wa siku nne na hivyo kuisababisha mamlaka hiyo hasara ya Dola za Marekani 600,000  (Sh. milioni 972).


Mkurugenzi Mtendaji wa Tazara, Ronald Phiri, alitangaza jana jioni kufukuzwa kazi wafanyakazi hao wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Phiri alisema amelazimika kuchukua uamuzi huo kutokana na Tazara kupata hasara ya Dola za Marekani 150,000 kwa siku sawa na Dola 600,000 kwa siku nne walizogoma.

Alisema wafanyakazi waliofukuzwa kazi ni wa upande wa Tanzania tu ambao kutoka makao makuu ya Tazara idadi yao ni 826, Mkoa wa Dar es Salaam 120, Mkoa wa Mbeya 53, stesheni ya Kongolo Quarry ni 63 na idara ya Ujenzi ni watano.

“Wafanyakazi waliogoma ni upande wa Tanzania tu, lakini wa Zambia hawakugoma, watapewa barua rasmi za kufukuzwa kazi lei,” alisema Phiri ambaye ni raia wa Zambia.

Kutokana na kufukuzwa kazi wafanyakazi  1,076, watabakia wafanyakazi 312 kwa kuwa mamlaka ina jumla ya wafanyakazi 1,388.

Wafanyakazi hao walianza mgomo tangu wiki iliyopita wakishinikiza kulipwa malimbikizo ya mishahara ya miezi mitatu wanayodai tangu Mei mwaka huu.

CHANZO: NIPASHE

0 comments:

MSIMAMO WA LIGI KUU UINGEREZA

POS
LP CLUB P W D L GF GA GD PTS
1 (1) Chelsea 3 2 1 0 4 1 3 7
2 (2) Liverpool 2 2 0 0 2 0 2 6
3 (3) Tottenham Hotspur 2 2 0 0 2 0 2 6
4 (7) Manchester United 2 1 1 0 4 1 3 4
5 (4) West Ham United 2 1 1 0 2 0 2 4
6 (5) Southampton 2 1 1 0 2 1 1 4
7 (6) Manchester City 2 1 0 1 6 3 3 3
8 (8) Aston Villa 3 1 0 2 4 4 0 3
9 (9) Arsenal 2 1 0 1 4 4 0 3
10 (10) Stoke City 2 1 0 1 2 2 0 3
11 (11) Cardiff City 2 1 0 1 3 4 -1 3
12 (12) Fulham 2 1 0 1 2 3 -1 3
13 (13) Hull City 2 1 0 1 1 2 -1 3
14 (14) Everton 2 0 2 0 2 2 0 2
15 (15) Norwich City 2 0 1 1 2 3 -1 1
16 (16) Sunderland 2 0 1 1 1 2 -1 1
17 (17) West Bromwich Albion 2 0 1 1 0 1 -1 1
18 (18) Newcastle United 2 0 1 1 0 4 -4 1
19 (19) Crystal Palace 2 0 0 2 1 3 -2 0
20 (20) Swansea City 2 0 0 2 1 5 -4 0

0 comments:

CCM yamvua uanachama shemejiye Rais Karume

  Ni Mwakilishi na waziri wa zamani
Mwakilishi wa Kiembe Samaki (CCM) visiwani Zanzibar, Mansour Yussuf Himid.
Mwakilishi wa Kiembe Samaki (CCM) visiwani Zanzibar, Mansour Yussuf Himid, ambaye pia ni waziri wa zamani mwandamizi chini ya utawala wa Rais Amani Abeid Karume, amevuliwa uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mansour anayeelezwa kuwa ni shemeji yake na Rais Mstaafu Karume, alivuliwa uanachama huo na Halmashauri Kuu ya Taifa (Nec) ya CCM baada ya kusikiliza na kuridhia tuhuma dhidi yake kama zilivyokuwa zimekwisha kuamulia na Kamati Kuu Maalum ya Zanzibar iliyokaa chini ya Rais wa Zanzibar na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Dk. Ali Mohamed Shein, Agosti 16, mwaka huu.

Mansour anafikwa na masahibu hayo huku akielezwa kuwa yuko nyuma ya kikundi cha Uamsho kilichoanzishwa Zanzibar hivi karibuni na kuleta mzozo mkubwa wa kisiasa na kijamii.

Jana Katibu wa Nec wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye aliwaambia waandishi wa habari mjini Dodoma kuwa Mansour ametiwa hatiani kwa tuhuma kadhaa ikiwamo kukisaliti chama chake.

Kwa maana hiyo, jimbo la uchaguzi la Kiembe Samaki sasa litakuwa wazi kwani maamuzi hayo yanamfanya Mansoor kupoteza ujumbe wa baraza la wawalikishi.

Halmashauri hiyo pia imeridhia kung’olewa kwa makatibu wa jumuiya za chama hicho akiwamo Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Vijana (UVCCM), Martine Shigela.

Maamuzi hayo ya NEC ni utekelezaji wa mapendekezo yaliyotolewa na Kamati Kuu (CC) ya chama hicho.

Nape alisema Mansoor amevuliwa uanachama kutokana na tuhuma za kushindwa kusimamia malengo ya CCM na kutekeleza masharti ya uanachama.

Alitaja tuhuma ambazo Nec imejiridhisha nazo vya kutosha ni kushindwa kusimamia malengo ya CCM na kutekeleza masharti ya uanachama.

Nape alitaja tuhuma nyingine ni kushindwa kutekeleza wajibu wa mwanachama na kukiuka maadili ya kiongozi wa CCM.

Tuhuma nyingine ni kuikana Ilani ya CCM ya uchaguzi Mkuu wa CCM wa mwaka 2010-2015 na kuisaliti CCM.

“Kwa uamuzi huo wa kumvua uanachama wa CCM kwa hiyo siyo tena mwanachama na wala kiongozi wa chama cha Mapinduzi,” alisema.

Alisema kuwa Mansoor hawezi kukata rufaa kwa sababu hicho ni kikao cha mwisho kikatiba kwa kutoa maamuzi yanayohusiana na chama.

Kwa mara ya kwanza, tuhuma za Mansour zilifikishwa katika kikao cha Kamati ya Maadili ya CCM Zanzibar, kilichoketi Agosti 16, 2013 katika Ofisi za CCM Kisiwandui ambapo wajumbe wa kamati hiyo kwa kauli moja walitoka na azimio la kumfuta uanachama mwakilishi huyo.

Alidaiwa kushindwa kusimamia malengo, madhumuni na masharti ya chama.Aidha anadaiwa kutokusimamia wajibu wa mwanachama kwa kukiuka maadili ya kiongozi wa CCM, kwa kukiuka Ilani ya chama hicho ya mwaka 2010.

Hata hivyo, ilielezwa kuwa suala la kufukuzwa uanachama kwa mwakilishi huyo lilizua mjadala mzito katika kikao hicho, lakini baadaye wajumbe walikubaliana kwa kauli moja kufukuzwa kwake.

Mansoor amekuwa miongoni mwa Wazanzibari walio katika safu ya mbele kutetea muundo wa Muungano utakaoipa Zanzibar mamlaka kamili ya dola.

MANSOUR NI NANI HASA
Mansour aliteuliwa kuwa mjumbe wa baraza la wawakilishi na Rais Karume mwaka 2000 na kuteuliwa kushika wadhifa wa Naibu Waziri wa Maji, Nishati Ujenzi na Ardhi hadi mwaka 2005.

Mwaka 2005 alichaguliwa kuwa Mwakilishi wa Kiembe Samaki kupitia CCM, nafasi ambayo amedumu nayo hadi sasa. Mwaka huo aliteuliwa na Rais Karume kuwa Waziri wa Maji, Nishati Ujenzi na Ardhi hadi mwaka 2010.

Kati ya 2005 -2010 alikuwa Mweka Hazina wa CCM Zanzibar  wadhifa ulimpa fursa ya kuwa Mjumbe wa NEC na Kamati Kuu ya CCM. Mwaka 2010 hadi mwaka 2012, alikuwa Waziri wa Kilimo na Rasilimali.

Ilipofika 2009 alikuwa mstari wa mbele kuushutumu Muungano kuwa ni chanzo cha kudorora kwa Zanzibar huku akiendesha kampeni juu ya suala la mafuta kutokuwa la Muungano.
Katika uchaguzi wa mwaka jana ndani ya CCM, Mansour hakugombea nafasi yoyote ndani ya CCM.

Aidha, alihudumu kama mjumbe wa Baraza la Biashara la Zanzibar kati ya mwaka 2002 hadi 2012.

Kutokana na misimamo yake ndani na nje ya chama na Serikali, Oktoba 15, 2012, Dk. Shein ilifuta uteuzi wa Mansour kama waziri hivyo kubakia kuwa mjumbe wa Baraza la Wawakilishi hadi jana.

Mansour ni mwanasiasa na mfanyabiashara aliyezaliwa Novemba 3, 1967 kisiwani Unguja. Alisoma masomo yake ya msingi na sekondari nchini India kati ya mwaka 1976 na 1987.

Kabla ya kuingia rasmi katika siasa mwaka 2000, aliteuliwa kuwa mjumbe katika Baraza la Wawakilishi na alijihusisha katika biashara ya hoteli.

Mwanasiasa huyo ni mtoto wa Mkuu wa Kwanza wa Jeshi la Zanzibar baada ya Mapinduzi, Brigedia Jenerali Yussuf Himid.

Amekuwa akisimamia maridhiano ya Wazanzibari na Umoja wa Kitaifa akiwa mmoja wa wajumbe sita wa Kamati ya Maridhiano aliyoshiriki kikamilifu kuyaanzisha mwaka 2009.

Pia ni miongoni mwa Wazanzibari walio mstari wa mbele kutetea muundo wa Muungano, utakaoipa Zanzibar mamlaka kamili ya dola.

Wajumbe wengine wa Kamati hiyo ni Mwenyekiti Hassan Nassor Moyo (CCM), Eddie Riyami (CCM), Abubakar Khamis Bakari (CUF), Ismail Jussa Ladhu (CUF) na Salim Bimani (CUF).

Katika hatua nyingine Nec iliyokaa kwa siku tatu mjini Dodoma chini ya mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, pia kimeridhia uteuzi wa makatibu wa wapya wa Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), Jumuiya ya Wazazi na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT).

Katika uteuzi huo aliyekuwa Kaimu Katibu wa CCM Mkoa wa Morogoro, Sixtus Mapunda, ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa UVCCM Taifa, nafasi  iliyokuwa ikishikiliwa na Shigela.

Taarifa za zaidi kutoka Dodoma ambazo zimelifikia gazeti hili jana jioni, zinasema kwamba Seif Shabani Mohamed ambaye ni mjumbe wa NEC kutoka Pemba ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Jumuiya ya Wazazi nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Hamis Suleiman Dadi huku Amina Makilagi akiachwa kuendelea na nafasi yake ya Katibu Mkuu UWT.

Pia, NEC imeridhia mapendekezo ya CC ya kuziba nafasi za Makatibu wa CCM wa mikoa ya Morogoro, Kaskazini Pemba na Geita ambayo yamekuwa wazi kwa muda mrefu sasa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kifo.

Kutokana na hali hiyo, Romuli Rojas John ameteuliwa kuwa Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro. John kabla ya uteuzi huo alikuwa Msaidizi Kitengo cha Uchaguzi, Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM.

Aidha, Katibu wa CCM wilaya ya Mkinga mkoani Tanga, Kassim Mabrouk Mbarak, ameteuliwa kuwa Katibu mkoa Kaskazini Pemba wakati aliyekuwa Katibu wa CCM Wilaya ya Igunga ameteuliwa kuwa Katibu wa CCM mkoa wa Geita.

SAKATA LA MADIWANI BUKOBA

Kuhusu sakata la madiwani wanane wa Bukoba mjini waliotimuliwa na vikao vya CCM ngazi ya mkoa, Nape alisema kuwa suala hilo limeachwa kuendelea kushughulikiwa na kikao cha CC kilichokuwa kikiendelea jana usiku na kuahidi kutoa taarifa za maamuzi hayo leo.


Taarifa zaidi kutoka Dodoma zilieleza kuwa jana jioni baada ya NEC kumaliza kikao chake, wajumbe wa CC waliendelea kukutana na viongozi kadhaa wa CCM Mkoa wa Kagera akiwamo Mwenyekiti na Katibu wa Wilaya ya Bukoba.

Mapema jana kabla ya kikao cha NEC kuanza, Kamati Kuu ilikutana na Mbunge wa Bukoba Mjini, Balozi Khamis Kagasheki na Meya wa Manispaa ya Bukoba, Dk. Anatory Amani na kuwahoji na baadaye kuwahoji Mwenyekiti na Katibu wa CCM mkoa wa Kagera.

MSIMAMO WA CCM KUHUSU RASIMU YA KATIBA

Wakati Nape akiweka kiporo taarifa juu ya maamuzi yaliyofikiwa na Nec kuhusu Rasimu ya Katiba Mpya yaliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa ahadi ya kutolewa baadaye, habari zinasema mambo matatu mazito ya rasimu hiyo yamekataliwa.

Habari ambazo NIPASHE ilizipata kutoka Dodoma zinaeleza kuwa Nec imekataa suala la kuweka kikomo cha vipindi vitatu kwa wabunge.  Badala yake imependekeza mfumo wa sasa wa bila ukomo kuendelee.

Aidha, chama hicho kimekataa pendekezo la mawaziri wasitokane na wabunge na kutaka utaratibu wa sasa wa mawaziri kutokana na wabunge uendelee.

Kuhusu mfumo wa Muungano wa serikali tatu, CCM imepinga pendekezo hilo na badala yake kutaka mfumo wa serikali mbili uendelee kama ulivyo sasa.

Pendekezo ya Tume hiyo inayoongozwa na Jaji Joseph Warioba ya kuwa na uwakilishi wa asilimia 50 kwa 50 katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa wabunge wanawake na wanaume limekubaliwa na chama hicho tawala.
CHANZO: THE GUARDIAN

0 comments:

MATOKEO KAMILI YA LIGI KUU YA VODACOM: SIMBA YAVUTWA SHARUBU - YANGA YAUA, AZAM NA MTIBWA NGOMA DROO

Matokeo kamili ya Ligi Kuu Tanzania

Mtibwa Sugar 1 - 1 Azam FC
Rhino Rangers 2 - 2 Simba SC
Coastal Union 2 - 0 JKT Oljoro
Mbeya City 0 - 0 Kagera Sugar
Ruvu Shooting 3 - 0 Tanzania Prisons
Young Africans 5 - 1 Ashanti Unite

0 comments:

Tozo la simu kujadiliwa bungeni latoweka

Tegemeo la umma kwa serikali kuwasilisha bungeni muswada wa mabadiliko ya sheria iliyoanzisha tozo la Shilingi 1,000 kwa mwezi kwa watumiaji wa simu za kiganjani, limetoweka.

Hali hiyo inatokana na Bunge kupanga ratiba ya shughuli zake kwa Mkutano wa 12 unaoanza Jumanne wiki ijayo mjini Dodoma, pasipo kuwapo muswada wa mabadiliko ya Sheria ya fedha inayoanzisha tozo za simu.

Viongozi kwa nyakati tofauti wamekuwa wakinukuliwa wakisema kuwa suala hilo litarejeshwa Bungeni kujadiliwa upya baada ya kulalamikiwa na wananchi ambao wanapinga kodi hiyo mpya.

Hata hivyo, rasimu ya ratiba ya mkutano wa 12 wa bunge utakaoanza wiki ijayo, ambayo NIPASHE imeiona imeonyesha miswada itakayojadiliwa ni saba huku suala la kodi ya simu likiwa halijawekwa kabisa kujadiliwa katika mkutano huo.

Wakati wa mkutano wa bajeti la Bunge uliomalizika Juni mwaka huu, Bunge lilipitisha sheria ya fedha inayoanzisha kodi kwenye Kadi ya simu ambayo kila mtumiaji simu, bila kujali matumizi yake  atakuwa analipa Sh. 1,000 kwa mwezi.

Baada ya kupitishwa kwa kodi hiyo ambayo pendekezo lake lilitolewa na Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa  wakati anasoma hotuba yake ya Bajeti, utekelezaji wake ulipangwa kuanza Julai mosi, mwaka huu.

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa, akizungumza na NIPASHE jana alisema suala hilo kwa sasa linashughulikiwa na Idara ya Hazina iliyopo  Wizara ya Fedha.

“Tumeshakubaliana suala hili lishughulikiwe na Hazina, kwa hiyo halipo tena kwenye Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia,”alisema Profesa Mbarawa.

Kwa upande wake, Waziri wa Fedha Dk. Mgimwa alipoulizwa alisisitiza kuwa uamuzi wa kurejesha suala hilo bungeni upo pale pale hata kama rasimu ya ratiba ya mkutano wa 12 imeshatolewa.

“Kilichofikiwa hivi sasa ni kulifikisha suala hilo bungeni, katika mkutano utakaoanza wiki ijayo,”alisema Dk.Mgimwa.

Waziri huyo alipoulizwa kama uamuzi wa serikali ni huo kwanini suala hilo halijapangwa kujadiliwa katika mkutano wa 12 unaoanza wiki ijayo, alisema utaratibu uliopo ni kwamba kabla ya bunge kuanza vikao vyake Kamati ya Uongozi ya Bunge hukaa kujadili mambo ya kujadiliwa bungeni.

Wakati msimamo wa serikali kuhusu suala hilo ukiwa hivyo, rasimu ya ratiba ya mkutano wa 12 wa bunge iliyotolewa na Kamati ya Uongozi ya Bunge, imeonyesha pamoja na mambo mengi miswada itakayojadiliwa ni saba kuanzia Agosti 27 hadi Septemba 13, mwaka huu bunge hilo litakapoahirishwa.

Ratiba hiyo inaonyesha kuwa muswada wa sheria ya Tiafa ya umwagiliaji ya mwaka 2013 itajadiliwa, ukifuatiwa na muswada wa sheria ya takwimu wa mwaka 2013 utakaojadiliwa Agosti 29 mwaka huu.


Septemba 2, mwaka huu wabunge watajadili muswada wa sheria ya vyama vya ushirika wa mwaka 2013 na Septemba 4 mwaka huu, muswada wa sheria ya mfuko wa Akiba wa GEPF wa mafao ya wastaafu wa mwaka 2013.

Kwa mujibu wa ratiba hiyo, wabunge watapata fursa ya kujadili muswada wa sheria ya marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba wa mwaka 2013 Septemba 9 mwaka huu na mwisho watajadili muswada wa sheria ya kura ya maoni wa mwaka huu 2013.

Kutokana na ratiba hiyo, ni wazi kuwa suala la tozo la kodi za simu halitajadiliwa hali ambayo itaacha maswali mengi kwa wananchi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakilalamikia suala hilo litawaumiza watu wenye kipato kidogo.

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, akizungumza na wananchi wa mkoa wa Ruvuma Julai 21, mwaka huu alisema tozo hilo si ya kuwaumiza wananchi bali mapato yake yatakwenda moja kwa moja kusaidia kueneza umeme vijijini na kwamba wanaopinga hawatutakii mema.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Nchimbi asiponasa matajiri dawa za kulevya ajiuzulu-CUF

Baraza kuu la uongozi wa Taifa la Chama cha Wananchi (CUF), linamtaka Waziri wa Mambo ya ndani ya Nchi,  Dk. Emmanuel Nchimbi kujiuzulu kama atashindwa kuwakamata na kuwawajibisha matajiri wakubwa wanaofadhili mitandao ya biashara ya  madawa ya kulevya.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, wakati akielezea maazimio yaliyoamuriwa na kikao cha  Baraza Kuu la Uongozi la chama hicho.

Profesa Lipumba alisema kuwa anampongeza Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, kwa kubeba majukumu yaliyotakiwa yafanywe na Waziri wa Mambo ya Ndani  ya Nchi.

“Waziri Mwakyembe ana majukumu mazito ya kusimamia reli, bandari na viwanja vya ndege, usafirishaji na uchukuzi na kusikitishwa na uzembe unaofanywa na Jeshi la Polisi chini ya usimamizi wa mambo ya ndani kwa kushindwa kusimamia na kuwakamata watu wanaojihusisha na biashara haramu ya dawa za kulevya,” alisema.

Alisema bila aibu serikali inachukua hatua ya kumfukuza kazi askari polisi mwenye cheo cha koplo kwa kusaidia kupitisha madawa bila kuzingatia ukweli, na kudai kuwa koplo huyo alitumwa na vigogo kutoka serikalini.

“Serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM) ipambane na mapapa wa utoroshaji wa nyaraka za serikali na madawa ya kulevya badala ya kufanya geresha ya kupambana na vidagaa wa biashara hizi ambazo hata wakichukuliwa hatua kali bado wakubwa wa biashara hii wanaendelea kuliangamiza taifa,” alisema.

Aidha, alisema  Baraza Kuu  linamtaka Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile, ajiuzulu kwa uzembe wa kupigwa risasi Sheikh Ponda Issa Ponda na pia kupisha uchunguzi wa tukio hilo na kama hatafanya hivyo, serikali imwajibishe kwa lazima.


Aliongeza kuwa baraza linalaani kitendo cha kikatili cha kupigwa risasi kwa Sheikh Ponda.

“Sheikh huyu alipigwa risasi bila sababu, kwani hakuwa akipambana na polisi na wala hakuwa na silaha yoyote, hivyo baraza linaitaka serikali kuunda tume huru itakayochunguza suala hili kama zilivyoundwa tume huru nyingine kwenye matukio kadhaa ya uvunjwaji wa haki za binadamu.”

Aliongeza kuwa baraza linasikitishwa na kufedheheshwa na mgogoro wa kiuchumi uliotangazwa na nchi jirani za Rwanda na Uganda kuhusu kutotumia Bandari ya Dar es Salaam kwa sababu ya ubabaishaji unaofanywa na vyombo vya dola kama vile jeshi la polisi na askari wa usalama barabarani.

Alimtaka Rais Jakaya Kikwete kutafuta njia za kidiplomasia ili kuweza kutatua mgogoro wa kisiasa baina ya Tanzania na Rwanda ili kuleta maelewano ambayo yatadumisha mahusiano na usalama baina ya nchi hizi.

CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Kamati ya Bunge yabaini ufisadi Wizara ya Magufuli

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), imesema kuwa taarifa ya matumizi ya fedha katika Wizara ya Ujenzi, ina shaka kwani kuna  fedha ambazo ziliombwa kwa ajili ya miradi ambayo haipo.

Hayo yalibainishwa jana katika kikao cha kamati hiyo pamoja na watendaji kutoka Wizara ya Ujenzi.

Gaudence Kayombo, ambaye alikuwa mwenyekiti wa kikao hicho cha kamati  kilichofanyika jana katika ofisi ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam, alisema baada ya kupitia taarifa ya wizara hiyo, waliona kuna  Sh. bil. 348 ambazo ziliombwa na wizara hiyo kwa mradi ambao hauonekani.

Alisema  katika hotuba ya bajeti ya wizara hiyo mwaka juzi, ilionyesha kwamba kiasi hicho cha fedha kiliombwa kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara na siyo kama ilivyoelezwa kwenye taarifa iliyopitiwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na kamati hiyo.

Kayombo alisema kuwa, katika taarifa hiyo iliyoletwa mbele ya kamati hiyo ilieleza kuwa sehemu ya kiasi hicho cha fedha kilitumika kwa ajili ya kuwalipa makandarasi ambao wanawadai tofauti na maelezo yaliyopelekwa bungeni katika kipindi hicho.


Akijibu hoja hiyo, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Herbert Mrango, alisema kuwa, katika kiasi hicho walichoomba, bunge lilipitisha  Sh. bil. 253  na kwamba kati ya hicho kilitumika kuwalipa makandarasi hao ambao wanaidai wizara hiyo kwa madai ya kwamba wanapolipwa, kazi ya ujenzi wa barabara inakwenda haraka.

Hata hivyo, wajumbe wa kamati hiyo waliihoji wizara hiyo kwanini wanatumia fedha za serikali kinyume na taratibu za maelezo ya kibajeti yanayopelekwa bungeni.

Aidha, kamati hiyo iliitaka wizara hiyo kuonyesha wazi kiasi kamili cha fedha wanachoomba kwa ajili ya kulipia madeni wanayodaiwa na makandarasi wa barabara kwenye bajeti ya serikali wakati wa kuwasilisha hotuba ya bajeti ya wizara hiyo.

CHANZO: NIPASHE

0 comments:

soma majina ya wachezaji stars kuivaa Gambia............

Nyota 24 wakiwamo Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wa klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameitwa kuunda kikosi cha timu ya taifa (Taifa Stars) kitakachojiandaa kwa mechi ya kukamilisha ratiba ya Kundi C la kuwania kufuzu kwa fainali zijazo za Kombe la Dunia dhidi ya Gambia itakayochezwa Septemba 7, imefahamika.


Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Boniface Wambura, alisema jana kuwa wachezaji hao watatakiwa kuripoti kambini Agosti 29 kabla ya saa 1:00 usiku na siku inayofuata wataanza mazoezi kujiandaa kwa mechi hiyo.

Wambura alisema kuwa kocha wa Stars, Kim Poulsen, ambaye hivi sasa yuko England akiongeza ujuzi kwa kujifunza katika klabu ya Swansea inayoshiriki ligi kuu ya nchi hiyo, atarejea nchini Jumatatu (Agosti 26) kabla ya kuanza maandalizi ya mechi dhidi ya Gambia.

Aliwataja wachezaji walioitwa katika kikosi cha Stars kuwa ni makipa Juma Kaseja (huru), Mwadini Ali na Aishi Manula (wote Azam na Ally Mustafa 'Barthez' wa Yanga.

Mabeki ni Aggrey Morris na Erasto Nyoni (Azam), Kelvin Yondani, Nadir Haroub ' Cannavaro ' na David Luhende wa Yanga, Shomari Kapombe (Simba) na Vincent Barnabas (Mtibwa)

Viungo walioitwa kuitumikia Stars ni Khamis Mcha (Azam), Salum Abubakar (Azam), Said Dilunga (Ruvu Shooting), Frank Domayo (Yanga), Athuman Idd (Yanga), Haruna Chanongo (Simba), Amir Kiemba (Simba), Mrisho Ngasa (Yanga), Simon Msuva (Yanga), John Boko na Juma Liuzio (Mtibwa Sugar).

Katika mechu yao ya kwanza iliyiochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Stars ilishinda 2-1.

Ivory Coast wanaoundwa na nyota wanaocheza soka la kulipwa barani Ulaya kama Didier Drogba wa Galatasaray ya Uturuki na Yaya Toure wa Manchester City ya England wameshajihakikishia nafasi ya kufuzu kwa hatua ya mtoano baada ya kuwa na uhakika wa kumaliza kileleni mwa Kundi C, wakizipiku Morocco, Stars na Gambia.   
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Tambwe: Nitaipa Simba ubingwa

Mfungaji Bora wa michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati (Kombe la Kagame),  Mrundi Amissi Tambwe ameapa kujituma kwa uwezo wake wote na kushirikiana na wenzake ili kuipa taji la Ligi Kuu ya Tanzania Bara klabu yake mpya ya Simba.


Akizungumza na NIPASHE kwenye hoteli aliyofikia iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam jana jioni, Tambwe alisema ametua Simba kuisaidia kupata mataji hasa ubingwa wa Ligi Kuu ya Bara ambao hivi sasa unashikiliwa na mahasimu wao wa jadi, Yanga.

“Kazi ya straika (mshambuliaji) ni kufunga. Nimekuja Tanzania kuisaidia Simba kufunga magoli. Naamini nitaendelea kufunga magoli mengi kama nitapata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wachezaji wenzangu,” alisema Tambwe.

“Ligi ya Tanzania haitakuwa ngeni kwangu kwa sababu nawajua wachezaji wengi. Kina Cannavaro (Nadir Haroub), Yondani, Bocco… hawa wote nimekutana nao katika mechi za timu ya taifa,” aliongeza mshambuliaji huyo wa timu ya taifa ya Burundi.

Kwa upande wake, beki Gilbert Kaze, ambaye alikuwa na Tambwe katika hoteli hiyo, alisema amefurahi kutua katika timu yenye mashabiki wengi ndani na nje ya Tanzania na kwamba, anaamini hali hiyo itamsaidia kuimarisha kipaji chake kutokana na ushindani uliopo katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara kulinganisha na kwao (Burundi).

“Ligi ya Tanzania ni ngumu na inahitaji nguvu. Mimi ni mgeni na ligi ya nchi hii lakini nawajua baadhi ya wachezaji kama Kaseja, Nyosso, Nyoni na Kavumbagu … nawajua vizuri na nilishawahi kucheza nao,” alisema Kaze.

Tambwe na Kaze wameingia mikataba ya miaka miwili na Simba wakitokea klabu ya Vital'O ya Burundi, ambayo wametoka kuipa ubingwa wa Kombe la Kagame Julai mwaka huu.

Tambwe alisema jana kuwa alisainia mkataba Julai 7 mwaka huu wakati Kaze alikiri pia kumwaga wino wa kuichezea Simba Agosti 7. Mikataba ya wawili hao na klabu ya Vital'O itamalizika Septemba 27, siku ya kufungwa kwa msimu wa 2012/13 wa Ligi Kuu ya Burundi.
   
ZIARA KAHAMA
Katika hatua nyingine, Tambwe na Kaze leo wanatarajia kuondoka jijini Dar es Salaam kuelekea Kahama mkoani Shinyanga kuungana na wachezaji wenzao wa Simba ili kujiandaa na mechi yao ya ufunguzi wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara watakayocheza Jumamosi dhidi ya Rhino Rangers kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mkoani Tabora.

Katibu mkuu wa Simba, Evodius Mtawala, aliiambia NIPASHE jana kuwa tayari wameanza taratibu za kuwatafutia nyota hao vibali vya kuishi na kufanya kazi nchini kama taratibu zinavyoelekeza.

Mtawala alisema kuwa leo wanatarajia kutuma dola za Marekani 5,000 (Sh. milioni 8) kwa viongozi wa klabu ya Vital'O ya Burundi ili kukamilisha uhamisho wao wa kimataifa (ITC).

Kuwasili kwa wachezaji hao juzi usiku kunaifanya idadi ya wachezaji wa kigeni wa Simba kuwa wanne, wakiwamo kipa Abel Dhaira na beki wa kati Joseph Owino.

Endapo Simba itashindwa kukamilisha uhamisho wa Warundi hao hadi kufikia kesho (Alhamisi), wachezaji hao watashindwa kuitumikia timu hiyo katika mechi yao dhidi ya Rhino.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Dk. Mwakyembe awalipua Polisi

  Aeleza wamekalia kesi 36 za `unga`
Inspekta Jenerali wa Polisi, Said Mwema
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amehoji kesi 36 zinazohusiana na dawa za kulevya ambazo Jeshi la Polisi limekaa kimya kwa kutoeleza hatua zilipofikia, hali ambayo inatia shaka na kudhoofisha vita dhidi ya biashara hiyo haramu.

Alisema hayo juzi wakati akihojiwa na televisheni ya Channel Ten kuhusu serikali imejipanga vipi kukabiliana na biashara ya dawa za kulevya ambayo inaonekana kukithiri nchini na kuathiri asilimia kubwa ya vijana.

Dk. Mwakyembe alisema ili Watanzania wafahamu nini kinachoendelea kuhusiana na kesi hizo, ameahidi kuzifuatilia ikiwa ni mkakati wa kukabiliana na biashara hiyo.

“Nitazifuatilia hizo kesi kwa kumshirikisha waziri mwenzangu (Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi), ili tujue hizo kesi zimefikia wapi na pia je, tule (ile) tumifuko (mifuko) twa (ya) dawa za kulevya zimewekwa wapi? Tusije tukakuta kuna mchanga ndani yake,” alisema Dk. Mwakyembe.

Kuhusu baadhi ya vigogo kudaiwa kujihusisha na biashara hiyo, alisema kama yupo mtu ambaye anawafahamu kwa majina vigogo hao ampelekee taarifa kwani suala hili lilipofikia sasa halihitaji usiri.

Dk. Mwakyembe alisema wizara yake itawasiliana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ili balozi za Tanzania zilizopo nje, zianze kubana watu wanaojihusisha na biashara hiyo.

Kuhusu maofisa wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), waliodaiwa kula njama za kusafirisha dawa za kulevya kilo 150 zilizokamatwa nchini Afrika Kusini, alisema atashangaa iwapo atasikia kuwa wamepeleleza na ushahidi haujajitosheleza.

Alisema baada ya kuweka udhibiti katika viwanja vya ndege ambavyo vinatumiwa kuingiza na kusafirisha dawa za kulevya nchini, hatua inayofuata ni kubaini wanaowatuma watu wanaokamatwa wakisafirisha dawa hizo.

Alisema baada ya kuweka udhibiti katika viwanja vya ndege ambavyo vinatumiwa kuingiza na kusafirisha dawa za kulevya hapa nchini, hatua inayofuata ni kufanya utafiti watu wanaokamatwa wakisafirisha dawa hizo ni nani anayewatuma.

Dk. Mwakyembe alisema biashara hiyo itaweza kukoma tu iwapo mipaka yote itadhibitiwa kwa ushirikiano wa vyombo vya dola.

Agosti 15 mwaka huu, Dk. Mwakyembe aliwataja maofisa usalama wanne wanaodaiwa kuhusika katika njama za kusafirishwa kwa dawa za kulevya kutaka wafukuzwe kazi na kufunguliwa mashtaka ya jinai chini ya Sheria ya Kuzuia Dawa za Kulevya.

Dk. Mwakyembe aliwataja maofisa usalama hao watakaofukuzwa kazi na kufunguliwa mashtaka ya jinai chini ya Sheria ya Kuzuia Dawa za Kulevya kuwa ni Yusufu Daniel Issa, Jackson Manyonyi, Juliana Thadei na Mohamed Kalungwana.

Mbali na maofisa hao, pia aliliagiza Jeshi la Polisi kumwondoa mara moja katika uwanja huo, askari wake, Koplo Ernest na kumchukulia hatua za kinidhamu kwa kushiriki kwake kwenye njama za kupitisha mabegi sita ya dawa za kulevya, yaliyokamatwa nchini Afrika Kusini.

Pia alisema polisi inapaswa kumsaka Nassoro Said Mangunga aliyevikwepa vyombo vya dola nchini Afrika Kusini na kutoroka na mabegi matatu ya dawa hizo.

Dk. Mwakyembe alisema mbeba mizigo katika uwanja huo, Zahoro Mohamed Seleman, anapaswa kufukuzwa kazi, kukamatwa na kufunguliwa mashtaka ili kuunganishwa na wenzake kujibu mashtaka ya jinai.

Pia ameiagiza Idara ya Usalama wa Taifa kuendesha uchunguzi wa kina kwa maofisa wake waliokuwa zamu siku ya tukio, kwa kuchelewa kuwafikisha kwa mbwa wakati mwafaka kukagua mabegi hayo yaliyokuwa na dawa za kulevya na hivyo kuliletea Taifa fedheha kubwa.

Alisema ameamua kuchukua hatua hizo kwa kuwa tukio hilo siyo la kwanza, bali ni sehemu ya matukio mengi ya upitishaji wa dawa hizo katika uwanja wa JNIA, ambayo taarifa zake zinaifikia serikali pale watuhumiwa wanapokamatwa nje ya nchi wakitokea Tanzania.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Polisi: Mauaji bilionea wa Tanzanite ni kisasi

Wakati polisi mkoani Kilimanjaro wakitangaza kuwashikilia watu watatu kwa tuhuma za mauaji ya bilionea wa madini ya Tanzanite, Erasto Msuya (43), pia wamesema mauaji hayo ni ya kulipiza kisasi katika biashara ya madini.
Kauli hiyo ilitolewa mjini hapa jana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Robert Boaz, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari juu ya hatua waliyofikia katika kusaka waliohusika na mauaji hayo ambayo yalitetemesha miji ya Arusha na Moshi.

Msuya aliuawa saa 6:30 mchana kwa kupigwa risasi kando ya barabara kuu ya Arusha – Moshi eneo la Mijohoroni, wilayani Hai karibu na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), Agosti 07, mwaka huu na kufa papo hapo.

Alifika eneo hilo akiwa peke yake baada ya kupigiwa simu na watu anaowafahamu kwenda kufanya nao biashara inayohisiwa kuwa ni ya madini ya Tanzanite.

Jana Kamanda Boaz alisema kwamba watuhumiwa hao ambao ni wakazi wa mikoa ya Arusha na Manyara, walikamatwa juzi na kufanya mahojiano na makachero wa Polisi na watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Aliwataja waliokamatwa kuwa ni Sharifu Mohamed Athuman ambaye ni mchimbaji mdogo wa madini, Musa Juma Mangu ambaye ni dereva wa magari ya Shangarai mkoani Arusha na Shwaibu Jumanne Saidi, mkazi wa Mererani mkoani Manyara.

“Hawa tuliowatia mbaroni walikodishwa na wafanyabiashara waliokula njama za mauaji haya (hakuwataja wafanyabiashara hao), lakini tumefanya nao mahojiano na wakati wowote tutawaburuza kortini,” alisema Kamanda Boaz.

Kwa mujibu wa Kamanda Boaz, mauaji ya kikatili ya mfanyabiashara huyo yalisababishwa na kulipizana kisasi katika biashara ya madini.

“Inavyoonekana marehemu aliwekewa mtego na wauaji hao kwa kudai kwamba wana kiasi kikubwa cha madini na iko kama ni kulipizana kisasi kati yao ingawa tumewakamata watuhumiwa watatu,” alifafanua Kamanda huyo

Boaz alisema katika uchunguzi huo, wamefanikiwa kukamata pikipiki aina Toyo yenye namba za usajili T 316 CLV, ambayo ilitumika katika mauaji hayo ya kinyama.

Alisema uchunguzi zaidi juu ya mauaji hayo unafanyika na wahusika watafikishwa mahakamani taratibu za kuandaa mashtaka zitakapokamilika.

NIPASHE lilikuwa gazeti la kwanza kuelezea chanzo cha mauaji hayo ikiyafananisha na uhalifu unaofanywa na wahalifu wa kikundi cha mafia ambao huuana katika ama kudhumiana fedha au kulipizana kisasi katika biashara zao chafu.

Katika habari ambayo NIPASHE iliandika Agosti 9, mwaka huu yenye kichwa cha habari ‘Mauaji Bilionea Arusha ni biashara ya kimafia’ iliwanukuu baadhi ya wakazi wa jijini Arusha wakisema kuwa kuna kila dalili kuwa mauaji hayo ni matokeo ya kuzidiana kete katika biashara zisizo rasmi.

Habari hiyo pia iliongezewa nguvu na hoja ya watu wengi kwamba katika biashara ya madini ya Tanzanite usiri na kudhulumiana vimekuwa ni sehemu ya shughuli hiyo kiasi cha kusababisha visasi na hata mauaji.

“Wewe fikiria inakuwaje mtu abebe Sh. milioni 100 peke yake aende porini kote kule kufanya biashara.

Yaani anakwenda kununua madini porini, hana ulinzi, hana risiti hana nini… hapa aliitwa kuwa kuna mzigo kumbe wamemlengesha,” alisema mkazi mmoja wa Arusha ambaye aliomba kusitiriwa jina lake.

Aliongeza kuwa: “Unajua hawa wafanyabiashara bwana wana mambo yao mengi. Kwa sasa ni vigumu kusema hasa nini kimemtokea, lakini najua kwa miaka mingi mambo yao mengi ni deal (magendo) tu. Hata hapa unaona wazi kuwa maswali ni mengi kuliko majibu.”

Katika habari hiyo pia NIPASHE ilimnukuu mkazi wa Kaloleni Arusha anayejishughulisha na biashara ya utalii alisema kuwa ukiwaita wafanyabiashara wa madini wote hasa wenye vitega uchumi vikubwa jijini humo na kuwauliza nyaraka za shughuli za madini utashangaa kwa kuwa kila kitu kinafanyika kama watu wanaohama kesho.

“Si unajua bwana hata Benki Kuu ilikwisha kutoa maagizo kuwa hakuna malipo yanaozidi Sh. milioni 10 yanalipwa kwa cash (taslimu)? Sasa kama marehemu alikuwa na Sh. milioni 100 kama inavyoelezwa ina maana alikuwa anavunja sheria na pia anajihatarishia usalama wake mwenyewe,” alisema mkazi huyo huku akiomba jina lake lisitajwe kwa kuwa biashara za Arusha zina siasa zake.

Habari hiyo pia ilizungumza na kijana mmoja mkazi wa Usa River, Uria Nnko, ambaye amekuwa kwenye shughuli ya madini kwa kitambo sasa, ambaye alisema kuwa kwa muda mrefu sasa biashara ya Tanzanite jijini Arusha inategemea sana vijana aliosema “wanapiga mzigo” kutoka mgodi wa Tanzania One.

nko alisema kwa hali inavyoonyesha marehemu aliitwa kwenda kununua mzigo wa namna hiyo na kwa kuwa anajua hizo shughuli zipo aliingia kichwa kichwa kumbe safari hii alikuwa amewekewa mtego na waliomuua na kumpora.

Biashara hiyo imeelezwa kufanywa kwa mfumo wa uuzaji dawa za kulevya kama ambazo hufanywa duniani na makundi hatari ya uhalifu kama Mafioso (mafia) ambayo kila kitu humalizwa papo kwa papo bila nyaraka za kiserikali wala kibenki.


Kauli ya Kamanda Boaz sasa inathibitisha uvumi huu kwamba mauaji ya Msuya ni ya kulipizana kisasi katika biashara ya Tanzanite.
Msuya alifikwa na maafa hayo baada ya kudaiwa kupigiwa simu na watu waliotaka kumuuzia madini na kukubaliana wakutane eneo hilo.

Erasto alikuwa anamiliki mgodi wa Kalo uliopo Mererani na pia migodi mingine miwili ya baba yake Kikaango Msuya iliopo block B Mererani.

Mbali na migodi hiyo, Erasto alikuwa anamiliki vitegauchumi kadhaa ikiwamo hoteli moja kubwa inayojulikana kwa jina la SG Resort, iliyopo Sakina, Arusha.

CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Kizimbani kwa kukutwa na `unga`

Mfanyabiashara Edson Monyo (39) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, akikabiliwa na mashitaka  mawili ikiwamo kukutwa na dawa za kulevya zenye thamani ya Sh. milioni 68.

Mshtakiwa huyo alisomewa mashtaka yake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Hellen Riwa.

Wakili wa serikali Leonard Challo alidai kuwa Agosti 4, mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere alikamatwa na askari  akiingiza kilo 1,512.69 za dawa za kulevya aina   ya Heroin Hydrochloride zenye thamani ya Sh. 68,069,250.

Katika shtaka la pili ilidaiwa kuwa siku na tarehe ya tukio la kwanza mshtakiwa alikamatwa na askari akiingiza nchini dawa za kulevya aina ya bangi  yenye uzito wa gramu 34.77 yenye thamani ya Sh.13, 908,000.


Wakili Challo alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika.

Hata hivyo, Hakimu Riwa alisema mshitakiwa hatakiwi kujibu chochote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi ya dawa zenye thamani zaidi ya Sh. milioni 10.

Aidha, kesi hiyo upelelezi wake utakapokamilika itasikilizwa Mahakama Kuu Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam.

Mshitakiwa alikana shtaka la pili la kukamatwa akiingiza bangi nchini.
Hakimu Riwa alisema mshitakiwa apelekwe mahabusu hadi Septemba 3, mwaka huu, kesi hiyo itakapotajwa.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Mapapa wa madawa ya kulevya watajwa,soma majina yao wamo Morine Amatus Liyumba na mdogo wa Rostam Aziz

Gazeti la Jamhuri limeendelea kutaja majina ya wauza unga wiki hii likija na majina na matatu na makazi ya wahusika. Wapo waliotajwa kwa namba za magari yao.

Yapo majina 240, wako wahusika kutoka nchi za nje, lakini zaidi ya 95% ni watz

Miongoni mwao wamo Mdogo wa Rostam Azziz, aitwaye Assad Azziz (No 23 kwenye list) na mtoto wa Amatus Lyumba aliyekuwa BOT, Morine Amatus Lyumba(No 66 kwenye list)

Nimeyascan majina kutoka kwenye gazeti hapa chini:












Nawasilisiha. jamii mfolum
Source - Gazeti la Jamhuri.

0 comments:

msanii Dimond atajwa sakata la unga


*Utajiri, safari zake nje ya nchi vyatiliwa shaka
*Ahusishwa na mtandao hatari wa Masogange


KWA mara ya kwanza tangu lilipoibuka sakata la watu maarufu kujihusisha ama na utumiaji au usafirishaji wa dawa za kulevya, jina la mwanamuziki anayeaminika kuwa na ukwasi mkubwa kwa sasa hapa nchini, Nasseeb Abdulmaliki, maarufu zaidi kwa jina la Diamond, limeanza kutajwa kuwa ni miongoni mwa vigogo wa ‘unga.’

Tayari mjadala mkubwa wa chini chini umeibuka kwa watu mbalimbali wakiwemo mashabiki wake, na taarifa ambazo zimelifikia MTANZANIA Jumatano kutoka vyanzo mbalimbali zimedai kuwa, mwenendo wa maisha ya Diamond sasa unachunguzwa na baadhi ya maofisa wa vyombo vya dola vya ulinzi na usalama.

Kutajwa kwa jina la Diamond katika sakata hili, kunatiwa nguvu zaidi na mwenendo binafsi wa maisha wa msanii huyo maarufu wa muziki wa kizazi kipya, unaokwenda sambamba na ukwasi mkubwa alioupata katika kipindi kifupi.

Kama hiyo haitoshi, safari za nje ya nchi za mwanamuziki huyo unaohusisha ziara zake nchini Afrika Kusini na Uingereza, pia ni mambo ambayo yamechochea wingu la mashaka lililofikia hatua ya jina lake kuingizwa katika mtandao huo ambao katika siku za karibuni, umewagusa pia baadhi ya watu wenye majina makubwa katika jamii.

Kuhusu ziara hizo, kilicholeta mshtuko na dukuduku dhidi yake ni kuwapo kwa taarifa kwamba, katika moja ya ziara hizo za nje ya nchi, Diamond alifikia hatua ya kusafiri akitumia chumba kinachotumiwa na wageni mashuhuri (VIP), badala ya njia ya wasafiri wa kawaida.

Mbali na hilo, taarifa nyingine zinaeleza kwamba, mizigo ya msanii huyo ambaye mara kadhaa amekuwa akisafiri na kundi la wacheza shoo wake, imekuwa ikipita pasipo kupitishwa katika hatua za ukaguzi kwa namna ile ile ilivyokuwa kwa mabinti wawili wa Kitanzania walionaswa nchini Afrika Kusini baada ya kuruka mfumo wa ukaguzi wa JNIA.

Aidha, ukaribu wa kimahusiano kati ya Diamond na baadhi ya Watanzania wanaoishi nchini Afrika Kusini na ambao majina yao pia yameanza kuhusishwa na biashara hiyo ya mihadarati, ni jambo jingine ambalo limechochea harakati za kufuatiliwa kwa karibu kwa nyendo za Diamond.

Taarifa zaidi kutoka JNIA zinaeleza kwamba, miongoni mwa watu wanaoweza wakawa wamemponza Diamond ni wale ambao walionekana kuwa karibu na Agness Gerald ‘Masogange’ (25) na Melisa Edward (24), siku walipokuwa wakisafiri kwenda Afrika Kusini kabla hawajanaswa katika uwanja wa Ndege wa Oliver Thambo jijini Johannesburg nchini Afrika Kusini, wakiwa na shehena ya dawa za kulevya.

Mwenendo wa watu hao unatiliwa shaka kuwa huenda ni miongoni mwa wafanyabiashara wakubwa wa dawa za kulevya wenye maskani yao nchini Afrika Kusini, kwa sababu mbali na ukaribu na wasichana hao, pia walihusika kwa karibu kuusafirisha mwili wa mwanamuziki Albert Mangwair, aliyefia huko huko Afrika Kusini ambaye taarifa za kufa kwake ziligumbikwa na matumizi ya dawa za kulevya.

Alipoulizwa jana na MTANZANIA Jumatano kupitia simu yake ya kiganjani kuhusu taarifa hizo na iwapo amekwishahojiwa na vyombo vya dola baada ya jina lake kuanza kutajwa kuwa miongoni mwa orodha ya wasanii wa muziki wanaosafirisha dawa za kulevya, Diamond alikiri kuwa na pesa za kutosha kuishi maisha anayoyataka, lakini akakana kujihusisha na biashara hiyo.

Akifafanua tuhuma moja baada ya nyingine kwa mpangilio aliokuwa akiulizwa na gazeti hili, Diamond alisema katika maisha yake, hajawahi kujihusisha na utumiaji au usafirishaji dawa za kulevya, lakini madai hayo yamekuwa yakitolewa dhidi yake na watu ambao hawajui siri ya mafanikio yake.

“Kazi ngumu siku zote inalipa, sasa napata matunda ambayo yanatokana na kile nilichokifanya, iweje watu wanitilie mashaka, Watanzania ni mashahidi wangu wananiona navyochumia juani, nitaendelea kulia kivulini tu kwani nakula kwa jasho langu.

“Siyo kweli kwamba mizigo yangu haikukaguliwa na kama haikukaguliwa na ingekuwa na kasoro, basi Uingereza wangenitia hatiani, nilipita na nilikaguliwa.” Alisema Diamond.

Alipoulizwa kuhusu taarifa za kuwa mwanamtandao wa kundi la Masogange, pia alikanusha kwa kueleza kuwa hata siku aliyosafiri kwenda Afrika Kusini alikwenda peke yake uwanja wa ndege na kuongeza kuwa alikwenda huko kwa shughuli za kimuziki, ambapo safari nzima iligharimu zaidi ya Dola 30,000 za Kimarekani.

“Afrika Kusini nimekwenda kufanya kazi zangu na safari hiyo imenigharimu zaidi ya Dola 30,000, nilikwenda kurekodi nyimbo yangu mpya inayoitwa namba moja ambayo itaanza kusikika hivi karibuni.

“Unajua Watanzania sasa hivi wanajua mtu hawezi kufanikiwa au kupata maendeleo bila kuuza ‘unga’, hili si sawa juhudi za mtu ndizo zinamfikisha alipo, na mimi juhudi zangu ndio zinanifikisha hapa, watu waache kunijadili vibaya.” Alisema Diamond.

Kuibuka kwa taarifa hizi kumekuja ikiwa ni takribani miezi miwili sasa tangu Watanzania wawili, Agness Gerald ‘Masogange’ (25) na Melisa Edward (24), waliokuwa na uhusiano wa karibu na baadhi ya wanamuziki maarufu hapa nchini, kukamatwa nchini Afrika Kusini wakiwa na dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani ya Sh bilioni 6.8.

Mbali na kuwa na uhusiano wa karibu na wanamuziki, Edward anadaiwa kuwa alikuwa mfanyakazi katika mgahawa mmoja maarufu jijini Dar es Salaam, unaomilikiwa na mmoja wa vijana matajiri hapa nchini ambaye hata hivyo gazeti hili halijafanikiwa kumpata ili kufanya naye mahojiano.

Wakati huo huo, tayari hatua za kinidhamu zimekwishaanza kuchukuliwa dhidi ya wafanyakazi wa JNIA waliohusika kupitisha kilo 150 za dawa za kulevya, ambao Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, ametaja majina yao hivi karibuni na kuonyesha kwa waandishi wa habari ushahidi wa kuhusika kwao.


CHANZO: Gazeti la Mtanzania - Agosti 21, 2013

0 comments:

download new trak..stereo-haina ngwasu

 click hyo link ku download
http://www.hulkshare.com/qp33lrvw87wg

0 comments:

unyama:Wanawake wachinjwa na kuchomwa moto

Mama na mwanae wameuawa kikatili baada ya kukatwa mapanga na baadhi ya viungo vyao kuchomwa moto katika tukio linalohusishwa na imani za kishirikina lililotokea mkoani Shinyanga.
Wanawake hao vikongwe mtu na mtoto wake ni Jadi Temi (90) na mwanae Samara Mathias (70) wakazi wa kijiji cha Ikonda wilayani Shinyanga.
Wawili hao walishambuliwa na kuuawa juzi na watu wasiojulikana wakiwa wamekaa nje ya nyumba yao wakiota moto na kufurahi chakula cha usiku.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinha Kihenya Kihenya, alisema vikongwe walishambuliwa na mapanga sehemu mbalimbali za miili yao na kufa papo hapo huku baadhi ya viungo vya Samara vikitupwa kwenye moto uliokuwa jirani.
Kihenya alisema tukio hilo lilitokea Ijumaa saa 2:00 usiku katika kijiji cha Ikonda wilayani Shinyanga, wakati wawili hao wanaoishi peke yao wakila chakula na kuota moto.
Kihenya alifafanua kuwa mara baada ya kushambulia na kuua wauaji hao wakikata kichwa cha Samara, kiganja cha mkono wa kushoto na mguu wa kulia na kuvitupa kwenye moto uliokuwa jirani .
Alisema wauaji hawakuiba chochote na kuna wasiwasi kuwa mauaji hayo yamefanywa kutokana na ushirikina .
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

PATA MATOKEO ZA LIGI DUNIANI(mechi za jana)


England - Premier League ‎(ENG)‎
Premier League
Full time
Liverpool Stoke
Spain - Primera Division ‎(ESP)‎
Primera División
1. Bundesliga ‎(GER)‎
Bundesliga 2013-2014
France - Ligue 1 ‎(FRA)‎
Regular
International Friendlies ‎(INT)‎
International Friendlies 2013
Italy - Coppa Italia ‎(ITA)‎
Third Round
Full time
Livorno Siena
Full time
Trapani Padova
Full time
Torino Pescara
Full time
Reggina Crotone
Full time
Avellino Cesena
Full time
Chievo Empoli
Full time
Bologna Brescia
Full time
Sampdoria Benevento
Full time
Sassuolo Novara
Full time
Cagliari Frosinone
Full time
Parma Lecce
Portugal - Premier League ‎(POR)‎
Regular Season
Netherlands - Eredivisie ‎(NED)‎
Full time
RKC AZ
Greece - Super League ‎(GRE)‎
Full time
PAOK Xanthi
Russia - Premier League ‎(RUS)‎
Premier League 2013–14
 

0 comments: