Mzozo kati ya Cisse na klabu yake umetatuliwa

 
Papiss Cisse na wasimamizi wa klabu ya Newcastle hatimaye wameafikiana na sasa mchezaji huyo ataanza kuvalia sare rasmi ya klabu hiyo iliyo na nembo ya kampuni ya Wonga, licha ya msimamo wake wa kidini.
Cisse, ambaye ni Muislamu, alijiondoa kutoka kwa kikosi cha Newcastle kilichokwenda ngambo kwa mazoezi yake ya klaby ya msimu kuanza, baada ya kuwafahamisha wasimamizi wa klabu hiyo kuwa hakuwa tayari kuvalia sare ambayo inaendeleza kampuni ya kutoa mikopo.
Lakini baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa muda wa wiki moja, pande hizo mbili zimeafikiana na Cisse sasa ataendelea kuichezea klabu hiyo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka ishirini na minane anatarajiwa kurejea tena katika kambi ya Newcastle baada hii leo.
Cisse ni mmoja wa wachezaji wa Newcastle ambao ni Waislamu lakini ndiye mchezaji wa pekee ambaye alikataa kuvalia sare hiyo.
Nyota huyo wa timu ya taifa ya Senegal amekuwa akifanya mazoezi mwenye huku wachezaji wenzake wakiendelea na mazoezi yako nchini Ureno.
Oktoba mwaka uliopita, ilitangazwa kuwa kampuni inayotoa mikopo kwa riba ya juu ya Wonga, itakuwa mdhamini mkuu wa klabu hiyo msimu huu kuchukua mahala pa kampuni ya kutuma pesa ya Virgin.
Inaaminika kampuni kugharimu dola milioni nane.
Cisse alijiunga na Nedwcastle Januari mwaka wa 2012 na amefunga jumla ya magoli ishirini na sita

0 comments:

Wahitimu wa vyuo vikuu kuwezeshwa mikopo kujiajiri


Wizara ya Kazi na Ajira kwa kushirikiana na Benki ya CRDB imezindua mpango wa kukuza ajira kwa vijana 30,000 kwa kuwapatia mikopo wahitimu wa vyuo vikuu vya elimu ya juu.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa wizara hiyo Ridhiwani Wema, alisema lengo la mpango huo ni kuongeza idadi ya vijana wanaomiliki shughuli rasmi za kiuchumi na waweze kujiajiri na kuajiri wengine na kukuza utamaduni wa kijasiriamali pamoja na ubunifu.

“Serikali imeamua kutoa fursa kwa vijana 30,000 za moja kwa moja kwa wahitimu wa elimu ya juu kwa kipindi cha miaka mitatu na kuwawezesha wenzao wa kada ya uchumi wasiopungua 100,000, ajira hizi zitakuwa ni za moja kwa moja mbali na zile zitakazotokana na mnyororo mzima wa thamani” alisema Wema.

Alisema serikali imekubaliana na benki ya CRDB kuanzisha utoaji wa mikopo kwa vijana mara utekelezaji wa program utakapoanza.

Pia alisema kuwa mpango huo  utatekelezwa na serikali kwa kushirikiana na vyuo vya elimu ya juu nchini, taasisi za fedha na wabia wa maendeleo.

CHANZO: NIPASHE

0 comments:

IDDY AZZAN ASEMA "Nipigwe risasi au ninyongwe hadharan"

Mbunge wa Kinondoni(CCM),Idd Azzan
Wakati Jeshi la Polisi likitoa visingizio kwamba linashindwa kunasa watuhumiwa wanaosafirisha dawa za kulevya wanaopitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), kutokana na kukosekana kwa vitendea kazi, Mbunge wa Kinondoni (CCM), Idd Azzan, amesema yupo tayari kupigwa risasi au kunyongwa hadharani kama itathibitika anahusika na biashara hiyo.

Azzan alitoa kauli hiyo jana wakati akihojiwa na kipindi cha Kumepambazuka kinachorushwa na Radio One kuhusu kuwapo kwa madai ya barua iliyoandikwa na Mtanzania aliyefugwa Hong Kong nchini China akimtaja kuhusika na biashara ya dawa hizo.

Alisema hahusiki kwa namna yoyote ile na biashara ya dawa za kulevya au biashara yoyote haramu na kwamba taarifa zilizoandikwa kwenye mitandao ya kijamii ni za upotoshaji na zimetolewa kwa lengo la kumchafua.

 “Nimejipeleka polisi kwa mara nyingine tena na nimewaomba wafanye uchunguzi wa kina na kama nitabainika nahusika na biashara hiyo niko tayari kupigwa risasi hadharani, lakini pia sitendewi haki kwa wale ambao wanazusha jambo hili wachukuliwe hatua za kisheria,” alisema.
 Azzan aliongeza kuwa hayupo juu ya sheria hivyo ikithibitika kuna mtu anamtuma dawa za kulevya kupitia bandari fulani pia atakuwa tayari kuwekwa hadharani na kunyongwa maana atakuwa hafai kuendelea kuwapo Tanzania.

Alisema makundi yanayomwandama ni ya kisiasa kwa lengo la kutaka kumdhoofisha katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015.

Mahojiano kati ya Azzan na radio yalikuwa kama ifuatavyo;

RADIO: Mhe Idd Azzan wewe ni mbunge wa Kinondoni inaelezwa kuwa wewe ni mmoja kati ya watu wanaojihusisha na dawa za kulevya na mmekuwa mkipokea mizigo kupitia maboti makubwa yanayotoka Pakistan yanayopitia Bagamoyo, Tanga, Mtwara na Dar es Salaam, hebu tujuze na wajuze Watanzania hili lina ukweli gani.

AZZAN: Hata mimi nimesikia hilo na bahati nzuri nimesoma kwenye mitandao kadhaa imeandika hivyo na kuna barua inayodaiwa kuandikwa na mfungwa mmoja ambaye amedai mimi ndiye nahusika kumtuma yeye.
 Napenda kuwajulisha Watanzania sihusiki kwa namna yoyote ile na biashara ya dawa za kulevya na siyo dawa za kulevya tu lakini pia biashara yoyote haramu sijawahi kufanya katika maisha yangu.

Niseme tu kuwa hizo ni taarifa ambazo zimetolewa kwenye mitandao ili kuaminisha watu hivyo, lakini kimsingi sihusiki na sijihusishi na biashara ya namna hiyo.

Baada ya kuziona habari hizi kwenye mitandao nilichokifanya na sababu ilishawahi kujitokeza tena na viongozi wangu wa CCM walishawahi kuyasema hayo kwenye mkutano wa vijana nikawaambia polisi wachunguze ili kupata ukweli wa hilo jambo.

Kama itabainika nahusika basi nichukuliwe hatua za kisheria mimi siyo Mungu wala sipo juu ya sheria, nimefanya hivyo kwa maana ya kuongea na Jeshi la Polisi nimejipeleka nimetoa maelezo na nimewataka polisi kwa sababu ni kazi yao wafanye uchunguzi wa kina, pili kama nahusika na tuhuma hizo hatua za kisheria zifuatwe dhidi yangu na kama siyo kweli hao wanaoeneza uzushi huo pia wachukuliwe hatua.

 RADIO: Unadhani kwa nini Mtanzania aliyeshikiliwa Hong Kong amekutaja wewe kuhusika na biashara hiyo?

AZZAN: Kwanza mimi siamini kwamba kuna Mtanzania anayeshikiliwa Hong Kong ambaye amenitaja mimi, sababu hiyo biashara kwanza sijawahi kuifanya, mimi niliiona hiyo barua haina jina la huyo Mtanzania mnayemsema, wala hakuna namba ya mfugwa sasa mfungwa anatakiwa kuwa na namba, asitaje jina ataje basi walau namba yake pia hakuna jina la gereza, kwa hiyo mimi siamini Mtanzania ambaye amefugwa kwa tuhuma za dawa za kulevya anitaje mimi kuwa nimemtuma. Hakuna hicho kitu na hakuna Mtanzania ambaye niliwahi kumtuma hicho kitu kimetengenezwa kwa nia ya kunichafua.

RADIO: Mheshimiwa unatafsiri vipi tukio hili?

AZZAN: Mimi ninachotafsiri tayari mapambano ya 2015 ndiyo yanaanza na watu wanatafuta jinsi ya kunichafua sababu hata tukienda kwenye kura nitawashinda, lakini si kutafuta mbinu chafu za kunichafua.

Yapo maneno ambayo nayazungumza bungeni hayawafurahishi wengine, lakini kwa Watanzania wengi yana manufaa, kwa hiyo kwa wale ambao hayawafurahishi wanaweza wakawa wamechangia katika kunichafua.

RADIO: Lakini Mheshimiwa Idd Azzan mara nyingi tu umekuwa ukitajwa na watu mbalimbali kwamba unajihusisha na uuzaji wa dawa za kulevya ama wewe ni mmoja kati ya watu wanaowaagiza watu mbalimbali kusafirisha mizigo hiyo ya dawa za kulevya hilo kwa upande wako unalizungumza vipi.

AZZAN: Nasema binafsi nimejipeleka polisi na nilishajipeleka mara ya kwanza baada ya kutokea tuhuma kama hizi, nikawaambia polisi wafanye uchunguzi kama nahusika nichukuliwe hatua za kisheria, nimekwenda tena kuwaambia polisi na nasisitiza polisi wafanye uchunguzi wa kina kama nahusika hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yangu.

Kama nitabainika nahusika na biashara hiyo niko tayari kupigwa risasi hadharani, lakini pia sitendewi haki kwa wale ambao wanazusha jambo hili wachukuliwe hatua za kisheria.

RADIO: Lakini Mheshimiwa kwa upande mwingine tayari taarifa zimeshatolewa kama hivyo kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii, sasa endapo itabainika kweli umehusika ama hujahusika ni kitu gani ambacho utakifanya.

AZZAN:  Naomba niweke wazi kama itathibitika ninamtuma mtu madawa ya kulevya kupitia bandari gani mimi nipo tayari kuhukumiwa sababu sipo juu ya sheria na pia nipo tayari niwekwe hadharani waninyonge sifai kuendelea kuwapo Tanzania kama nahusika na hilo, na kama sihusiki serikali initendee haki kwa watu wanaosambaza uvumi huu nao wachukuliwe hatua siyo wakae tu na kumrushia mtu vitu vya uongo.

Awali Kamanda wa Polisi Viwanja vya Ndege, Deusdedit Kato akihojiwa katika kipindi hicho juu kwanini JNIA umeonekana kuwa kitovu cha kupitishia dawa za kulevya, alisema sababu kubwa ni kwamba kuna tofauti kati ya nchi na nchi katika masuala ya teknolojia katika kubaini dawa za kulevya.

Kamanda Kato alisema nchi nyingine wana vifaa vya kisasa zaidi na kwamba wakati sasa umefika kwa serikali kuwekeza katika kupata vitendea kazi zaidi ili kufanikisha mapambano ya dawa za kulevya.

Aliongeza kuwa wamekuwa wakishirikiana na viwanja vingine vya nchi mbalimbali kwa kubadilishana taarifa lengo likiwa ni mapambano ya biashara hiyo.

“Kimsingi wanaokamatwa wanakuwa ni wabebaji tu na siyo matajiri wa dawa za kulevya, bahati mbaya wabebaji wamekuwa wagumu sana kutoa ushirikiano kwa polisi, nasisitiza vitendea kazi vinachangia kuponya mtu asikamatwe nchini na kwenda kukamatwa nje,” alisema.

 Kamanda Kato alisema katika kipindi cha miezi sita hadi nane watu 14 wamekamatwa wakituhumiwa kusafirisha dawa za kulevya nchini.

•Julai 5, mwaka huu wasichana wawili, Agnes Jerald (25) na Melisa Edward (24), walipita JNIA na shehena ya dawa za kulevya kilo 150  na walikamatwa Afrika Kusini na kushtakiwa nchini humo kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya.
 Hawa walikamatwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo wakiwa na shehena ya dawa hizo aina ya Crystal Methamphetamine zenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 6.8.

•Ijumaa wiki iliyopita yaani Julai 26, mwaka huu, Watanzania wengine wawili, walikamatwa Hong Kong wakiwa na dawa za kulevya aina ya cocaine na heroine zenye thamani ya Sh. bilioni 7.6 akiwamo mmoja aliyekamatwa akitokea Dar es Salaam kupitia Dubai hadi Hong Kong.

Taarifa kutoka Hong Kong za Ijumaa wiki iliyopita zinaeleza kwamba, maofisa ushuru wa Uwanja wa Ndege wa Hong Kong (HKIA), walimkamata kijana mmoja mwenye umri wa miaka 26 akitokea Tanzania na alikuwa na dawa za kulevya aina ya heroine kilo 1.6 zenye thamani ya Sh. bilioni 1.5, kwenye mzigo wake wa mkononi.

•Siku hiyo hiyo jioni, maofisa hao walimkamata Mtanzania mwingine mwenye miaka 45 ambaye alipelekwa hospitali na kutolewa gramu 240 za dawa za kulevya aina ya heroine. Taarifa zaidi zilieleza kuwa Mtanzania mwingine mwenye miaka 28 alikamatwa akiwa na kilo 2.03 za cocaine.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Serikali yasalimu amri kodi ya simu

Waziri wa Fedha, , Dk. William Mgimwa
Serikali sasa imekubali kuwa kodi mpya ya laini ya simu ni mgogoro na inakusudia kurejesha muswada wa sheria ulioazisha kodi hiyo bungeni kwa mjadala zaidi.

Waziri wa Fedha, , Dk. William Mgimwa, alisema jana alipozungumza na NIPASHE ofisini kwake jijini Dar es Salaam na mjadala huo unatarajiwa kufanywa wakati wa mkutano wa bunge unaotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi ujao.

Mgimwa alisema kwa sasa suala hilo linashughulikiwa kwa mapana zaidi na Serikali na linatarajiwa kupelekwa bungeni kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi zaidi.

Alisema wabunge watapata nafasi ya kujadili suala hilo na kueleza kuwa muafaka utapatikana katika vikao hivyo.

Wakati Dk. Mgimwa akitoa kauli hiyo, leo utaratibu wa makato ya laini za simu ya Sh. 1,000 unatarajia kuanza kwa kampuni zote za simu nchini.

Kodi hizo zilianza kutozwa na serikali mwanzoni mwa Julai, mwaka huu hivyo kuwalazimu wamiliki wa simu nchini kuingia gharama zaidi kwa asilimia 14.5 ili kuongeza mapato yake na kugharamia elimu.

Akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2013/14 bungeni Juni 13 mwaka huu, Waziri Mgimwa alisema kodi hizo zingeanza kutozwa Julai mosi mwaka huu.

Dk. Mgimwa alisema kuwa kama chanzo kipya cha mapato ya Serikali, inakusudia kutoza ushuru kwenye huduma zote za simu za mkononi badala ya muda wa maongezi peke yake.

Alifafanua kuwa asilimia 2.5 ya mapato ya kodi hiyo yatatumika kugharimia elimu nchini kwa kuzingatia mapendekezo ya Kamati Maalumu ya Spika ya Kushauri kuhusu mapato na matumizi ya Serikali.

Vilevile alitangaza kuanzisha kodi ya zuio ya asilimia 10 ya kamisheni ya usafirishaji wa fedha kwa njia ya simu za mkononi ambazo zitakusanywa na kampuni za simu kutoka kwa wakala wanaotoa huduma hizo kupitia simu za mkononi.

Kwa mujibu wa Waziri huyo, mapendekezo hayo ni utekelezaji wa ushauri wa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh kuwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), itafute vyanzo vipya vya kodi ili kuongeza mapato ya Serikali.

Wakati serikali ikiahidi kuchukua hatua hizo, tayari kodi hiyo imekabiliana na upinzani mkali kutoka makundi mbalimbali ya kijamii.

Miongoni mwake ni hatua zinazoratibiwa na Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, za kukusanya majina ya wananchi wasioitaka kodi hiyo pamoja na kuitisha maandamano ya kupinga kodi ya laini za simu.

Naye Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnahuye, naye amekuwa aliendesha kampeni ya kuipinga kodi hiyo.

 Hata hivyo, waliopitisha kodi hiyo ni wabunge wote wa CCM ambao walipitisha bajeti hiyo wakati wenzao wa Chadema wakiombolezwa vifo vya watu wanne waliuawa kwa mlipuko wa bomu katika mkutano wake wa kufunga kampeni za uchaguzi wa madiwani katika kata nne za Arusha Mjini.

Bomu hilo lilirushwa kwenye mkutano wa Chadema eneo la Soweto Juni 15, mwaka huu. Hadi sasa hakuna aliyekamatwa kwa ugaidi huo.

Wiki iliyopita Rais Jakaya Kikwete alikutana na Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Simu (MOAT) Ikulu kusikia pamoja na mambo mengine kodi ya simu itakavyokwaza maendeleao ya sekta ya mawasiliano, wakitaka serikali ifikirie kuondoa.

Hata hivyo, Rais Kikwete aliwataka MOAT kutoa mapendekezo ya jinsi serikali itapata kiasi cha Sh. bilioni 178 zilizopangwa kupatikana katika bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha wa 2013/14 kutokana na kodi ya simu.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

`Memory Card` yaleta hofu wakazi Butiama

Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Angelina Mabula
Aina mpya ya ukatili wa kijinsia maarufu kama `memory card' unaohusisha wanawake kuuawa na kunyofolewa sehemu za siri, imezua hofu miongoni mwa wakazi wa wilaya Butiama mkoani Mara.

Kati ya kipindi cha Desemba mwaka jana na Julai, mwaka huu, jumla ya wanawake 14 wanasadikiwa kufanyiwa ukatili huo.

Ukatili huo umebainishwa na wanawake mbalimbali walipokuwa wakizungumza kwenye mdahalo wa kupinga ukatili wa wanawake na watoto wa kike uliofanyika katika kijiji cha Bisumwa, Wilaya ya Butiama mkoani Mara ambapo walisema mauaji hayo yanaongozwa na kundi la watu wanaojiita makhirikhiri.

Mdahalo huo ambao uliandaliwa na shirika la kutetea haki za wanawake na watoto wa kike la Kivulini kupitia kampeni yake ya Tunaweza, wanawake hao walisema ukatili huo umekuwa ukifanywa na watu walio karibu na familia zao.

Kwa mujibu wa wanawake hao, katika kutekeleza ukatili huo, kundi hilo la makhirikhiri huwavizia wanawake wanapokwenda kuteka maji au wanapokuwa shambani na kuwavamia, kuwakata shingo na kisha kunyofoa kiungo katika sehemu za siri.

Mmoja wa wanawake hao, Maria Michael, alisema wauaji hao huchukua kiungo hicho pamoja na damu waliyokinga kutoka shingoni na kupeleka kwa waganga wa kienyeji kwa ajili ya kutengenezewa dawa ya kupata utajiri.

“Mauaji ya wanawake na kukatwa sehemu zao za siri pamoja na kichwa yamerudisha nyuma uchumi kutokana na wanawake hivi sasa kuhofia kutoka majumbani mwao kwenda kushiriki kazi za kiuchumi,” alisema.

Aliongeza kwamba huo ni ukatili ambao unapaswa kukomeshwa mara moja kwani hakuna uthibitisho wowote unaoonyesha kuwa kiungo hicho cha kike kinaleta utajiri.

Kwa mujibu wa Maria, vitendo hivyo vya ukatili vimesababisha wanawake kuungana katika makundi wanapokwenda kuteka maji au katika shughuli nyingine za kiuchumi ili kuepuka kuvamiwa na kundi hilo la makhirikhiri.

Akitoa mapendekezo ya nini kifanyike ili kukomesha mauaji hayo, Elizabeth Samson, aliwataka viongozi wa serikali za mitaa kuacha urasimu katika kushughulikia keso za ukatili wa kijinsia.

Aliongeza kuwa polisi pia wamekuwa wakichelewa kushughulikia kesi za ukatili wa kijinsia na baadhi yao hupokea rushwa na kuwaachia watuhumiwa.

Akielezea hatua zilizochukuliwa ofisa wa sera na utetezi katika shirika la Kivulini, Khadija Liganga, alisema mauaji hayo hufanyika kwa siri na polisi walithibitisha kuyafuatilia kwa karibu ili kubaini maeneo yanayoongoza.

Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Angelina Mabula, alisema hivi sasa matukio hayo yamedhibitiwa na serikali kwa kupitia kamati zake za ulinzi na usalama za wilaya na mkoa pamoja na kuimarisha ulinzi shirikishi.
 
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

TWITE CHINI YA UANGALIZI WA DOKTA

 
BEKI wa Yanga raia wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), Mbuyu Twite yupo chini ya uangalizi wa daktari bingwa, Gilbert Kigady wa Hospitali ya Trana Senta iliyopo Masaki, Dar es Salaam.Mchezaji huyo yupo chini ya uangalizi kutokana na uvimbe aliokuwa nao katika paja lake, baada ya kuumia wakati akiitumikia timu hiyo
. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi Dar es Salaam jana daktari wa Yanga, Nasoro Matuzia alisema bado hawajajua ni lini mchezaji huyo ataanza mazoezi."Kwa sasa tunaona maendeleo yake si mabaya tangu alipoanza matibabu kwa Dkt. Kigady, ila hatuwezi kusema lini ataanza kuitumikia timu," alisema Matuzia.
Aliongeza kuwa wanafanya jitihada za kumpatia matibabu mchezaji huyo kwa kuwa wanamtegemea katika kikosi cha Yanga.

0 comments:

Mwakyembe avutia pumzi `unga` airport


Kufuatia matukio mfululizo ya kukamatwa kwa watuhumiwa wa dawa za kulevya wanaodaiwa kuwa ni Watanzania kwenye viwanja vya ndege nje ya nchi wakipitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema atalishughulikia suala hilo kama alivyofanya bandarini.

Dk. Mwakyembe ambaye wizara yake ndiyo yenye dhamana na Mamlaka ya Viwanja vya Ndege nchini (TAA), alitoa kauli hiyo jana jijini Dar es Salaam wakati wa mazungumzo maalumu na NIPASHE kuhusu ufuatiliaji wa vitendo hivyo vinavyoharibu taswira ya nchi kimataifa.

Alisema anafahamu kila kitu kuhusu matukio ya dawa za kulevya, lakini anasubiri mamlaka zilizo chini yake kama vile TAA na bodi yake, uongozi wa JNIA na Polisi, ili wafurukute kwanza kama alivyofanya bandarini kwa lengo la kupima utendaji wao wa kazi.

“Mamlaka ni ‘system’, ina ngazi zake, kuna Mamlaka ya Viwanja vya Ndege na bodi yake, kuna polisi, kuna uongozi wa uwanja wa ndege. Nataka muwabane kwanza hao ili wawaeleze hayo (ma)dawa ya kulevya yanapitaje hapo? Mimi najua kila kitu kuhusu kinachoendelea na iwapo wanawazungusha njooni kwangu,” alisema Mwakyembe na kuongeza:

“Haiwezekani ukaenda moja kwa moja kwa Rais, iwapo kuna suala linalomhusu Waziri, atakushangaa na kukuona huelewi kitu. Najua hatua ilipofikia na iwapo kuna mamlaka haijachukua hatua yoyote, mimi nitaishughulikia. Na kama imepita kote na imefikia kwa DPP, najua imefika ngazi ya kiwizara, ni lazima tulishughulikie.”

Dk. Mwakyembe aliongeza kuwa, anajua mtandao wa dawa za kulevya ni mrefu, lakini atashughulikia kama alivyofanya katika Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), kwani baada ya kusikia ubovu unaotendeka aliwaacha wafurukute kwanza kwa takribani wiki mbili.

Alisema baada ya wiki hizo mbili akiwa na taarifa kamili kuhusu kilichokuwa kinaendelea, aliingia bandarini hapo na kuwafumua baadhi ya watendaji na kwamba ndivyo itakavyokuwa katika mamlaka zinazohusika na viwanja vya ndege kwani kwa sasa anasuburi kuona wanafanya nini kabla hajaingilia kati.

Agosti 27, mwaka jana, Waziri Mwakyembe aliunda Kamati ndogo ya Uchunguzi ya watu saba kubaini chanzo cha matatizo yanayozorotesha ufanisi katika Bandari ya Dar es Salaam na hivyo kukimbiwa na wateja wa ndani na nje ya nchi.

Baada ya uchunguzi huo, Dk. Mwakyembe aliwaondoa wajumbe wote wa Bodi ya TPA na kuteua wapya ili kuweka mazingira mazuri ya utekelezaji wa taarifa hiyo.

Juzi gazeti hili liliwasili katika ofisi za TAA, kwa lengo la kujua kinachoendelea kuhusu matukio hayo, lakini mmoja wa wafanyakazi katika ofisi hizo alisema Mkurugenzi wa mamlaka hiyo yupo, lakini asingeweza kuzungumza na waandishi bila kuruhusiwa kwanza na katibu wake wa mambo ya sheria, Ofisa Uhusiano na mwingine wa tatu ambao nao hawakuwapo hapo ofisini.

Mfanyakazi huyo wa kike ambaye alikataa kutaja jina lake wala cheo chake, alisema ofisi ya Mkurugezni ina watu watatu na utaratibu uliowekwa ofisini hapo ni kwamba, iwapo wafanyakazi hao wote hawapo, hakuna huduma itakayotolewa kwa mtu mwenye shida na Mkurugenzi kwa kuwa hataruhusiwa kumwona.

Hata hivyo, NIPASHE ilifanikiwa kumwona Mkurugenzi wa JNIA, Moses Malaki, ambaye naye alidai kwamba, hawezi kuzungumzia sakata hilo kwa madai kwamba hashughulikii masuala ya dawa za kulevya.

Malaki alisema wanaohusika na suala hilo ni polisi kwa kuwa JNIA wanahusika na masuala ya wasafiri na kwamba anayeweza kuzungumzia sakata hilo ni Mkurugenzi Mkuu wa TAA, Suleiman Suleiman.

Wakati wa mazungumzo na gazeti hili ofisini kwake siku hiyo, Malaki, alimpigia simu Suleiman ambaye aliahidi kukutana na NIPASHE jana saa 5 asubuhi ili kutoa ufafanuzi wa sakata hilo.

Hata hivyo, jana mwandishi wa habari hizi alikwenda ofisini kwa Mkurugenzi huyo na kutaarifiwa kwamba amsubiri kidogo kwa sababu yupo kwenye kikao.

Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa saa nne, katibu muhtasi wa mkurugenzi huyo alimweleza mwandishi kwamba bosi wake amekataa kuzungumzia jambo hadi atakapokuwa tayari.
"Mkurugenzi amesema hawezi kuzungumza tena na wewe hadi atakapopata muda wa kuongea na waandishi wa habari," alisema katibu ambaye hakutaja jina lake.

Kwa upande wake, Kamanda wa Polisi Kikosi cha Viwanja vya Ndege nchini, Deusdedit Kato, alisema kuwa, tayari wameshaandaa jalada la matukio hayo na juzi walilipeleka kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Hata hivyo jana, NIPASHE ilifika ofisini kwa DPP na kupewa taarifa ya kwamba yupo Dodoma kwa shughuli za kikazi hivyo msaidizi wake hawezi kuzungumzia lolote hadi yeye atakaporudi.
Julai 5, mwaka huu wasichana wawili wa Kitanzania walikamatwa nchini Afrika Kusini wakiwa na dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine kilo 150 zenye thamani ya Sh. bilioni 6.8,  zilizokuwa zikisafirishwa kutoka Tanzania.

Wasichana hao ambao ni Agness Gerald (25) na Melisa Edward (24), walikamatwa nchini humo katika Uwanja wa Ndege wa Oliver Tambo, uliopo eneo la Kempton Park.

Ijumaa wiki iliyopita, taarifa kutoka Hong Kong, zilieleza kwamba maofisa ushuru wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Hong Kong (HKIA), walimkamata kijana mwenye umri wa miaka 25 akitokea Tanzania akiwa na dawa na za kulevya aina ya heroine kilo 1.6 zenye thamani ya Sh. bil.1.5 kwenye mzigo wake wa mkononi.

Taarifa zinaeleza zaidi kwamba, maofsa hao jioni siku hiyo hiyo walimkamata Mtanzania mwingene mwenye umri wa miaka 45 ambaye alipelekwa hospitali na kutolewa gramu 240 za dawa aina ya heroine.

Mbali na hilo, pia Mtanzania mwingine mwenye miaka 28 alikamatwa akiwa na kilo 2.03 za cocaine.

Matukio hayo yametokea ikiwa ni takribani wiki moja baada ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Juni 28, mwaka huu kutangaza kuwa tatizo la dawa za kulenya hivi sasa ni janga la kitaifa.

Alisema kumekuwa na wimbi kubwa la Watanzania wanaojiingiza katika biashara haramu ya dawa za kulevya ndani na nje ya nchi na kwamba, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, watuhumiwa 10,799 walikamatwa kwa kujihusisha na dawa hizo.

Pia alisema katika kipindi hicho, Watanzania 240 walikamatwa katika nchi za Brazil, Pakistan na Afrika Kusini, na hivyo kuharibu taswira ya nchi na kusababisha Watanzania wasio na hatia kupata usumbufu na masharti magumu wanapotaka kusafiri kwenda nchi mbalimbali duniani.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

Usichokijua kuhusu Nash MC na maisha ya msoto aliyoyapitia hadi sasa kuitegemea sanaa, awaasa Ma-MC wasikurupuke



Nash MC ni moja kati wa wasanii ambao mara nyingi wamekuwa wakitajwa na wasanii wenzao kuwa wanaijua na kuifuata misingi ya Hip Hop, hata Madee wa Tip Top aliyewahi kusema kwenye wimbo wake ‘Hip Hop ina misingi nyie wabongo hamuiwezi’, aliwahi kutamka kwenye kipindi cha power jam kuwa mwana hip hop pekee anaemkubali Tanzania kwa kufuata misingi ni Nash MC.

Anajulikana kama Maalim Nash, na hivi sasa anataka afahamike kama Nash MC Palestina, kupitia ukurasa wake wa Facebook alifunguka undani wa safari yake ya muziki, misoto aliyoipitia na watu waliomsaidia hadi kufika hapa alipo anaitegemea sanaa.
“Wakati namaliza kidato cha 4 mwaka 2003 pale benjamin william mkapa,matokeo yalipotoka sikubahatika kufaulu wala kuendelea na elimu ya juu,na baba yangu mzazi alikua tayari ashafariki tangu mwaka 1999,M.a.p baba yangu,na hali za familia zetu mtaani nadhani wengi mnazijua pale unapomaliza shule jinsi unavyochukuliwa pale nyumbani kwenu.utaanza kuambiwa uchangie hela za mboga,unga na majukumu yanaibuka ghafla tu,nilijiuliza maswali mengi sana hivi nitaishi vipi????
Sikua na kazi wala kibarua na sanaa haikua imestawi katika upande wangu,kwa kweli hali ilikua ngumu sana,ila mwenyezi Mungu hakunitupa mja wake alinikumbusha kua kuna kipaji amenipa na nachotakiwa ni kukifanyia kazi kwa juhudi na maarifa sana,nililiona hilo na nikaanza kuzama katika utamaduni wa hip hop kwa nguvu na akili zaidi kwa muda wa miaka mi 5 au 6 nikawa nasoma na kujifunza mambo mengi sana juu ya hip hop kiundani mno sikukurupuka kwenda studio na baada ya hapo nikaanza kuonekana zaidi katika matamasha ya wapi na hatimae siku 1 nikapewa kipindi na saigon katika kituo cha eatv,na kuelezea hip hop na misingi yake na itikadi pia watu wengi walianza kunipenda na kunikubali sana na miaka miwili mbele nikakutana na mjomba Zavara na Lindu hawa walinipa miongozo mikubwa sana katika safari yangu na na wimbo wa kwanza kurekodi ilikua chini ya mtayarishaji Kita pale rama records,ulikua unaitwa, ‘nani mkali kwenywe game’ lakini ikumbkwe kua mwaka 2000.

0 comments:

WARAKA WA KALA KWA LOWASA


TANGAZO KWA UMMA

MIMI KALA JEREMIAH NILIKUWA MSANII WA KWANZA TANZANIA KUMSEMA MHESHIMIWA EDWARD LOWASA KUPITIA WIMBO WANGU UITWAO WIMBO WA TAIFA BAADA YA MHESHIMIWA KUKUMBWA NA KASHFA YA UFISADI WA RICHMOND.KWA KIPINDI KILE KILA MMOJA WETU ALIHAMAKI SANA NA KUONA KWELI MZEE WA WATU NI FISADI.KWENYE WIMBO HUO KUNA MISTARI NILISEMA. mi siyo mwana siasa sisubiri tume ichunguze nistaafu ka Lowasa.

KWA KUWA MIMI NI MZURI SANA KWENYE KUFANYA UCHUNGUZI BINAFSI NILITUMIA MUDA MWINGI SANA KULICHUNGUZA SWALA HILI LA KASHFA HII NA BAADAE NILIGUNDUA KUWA NI SWALA LA KISIASA.NA YALIKUWA NI MAPITO AMBAYO MWANADAMU YOYOTE HUPEWA MUDA WA KUPITIA MAGUMU ILI KUPIMWA IMANI YAKE KWA MUNGU.

BAADA YA KUGUNDUA HAYO MWAKA JANA NILITENGENEZA WIMBO UNAOITWA AZIMIO LA ARUSHA AMBAO UPO KWENYE ALBUM YANGU YA PASAKA AMBAYO IKO SOKONI TOKEA MWAKA JANA. KATIKA WIMBO HUO WA AZIMIO LA ARUSHA NILIANDIKA MISTARI IFUATAYO. walipiga dili waka msakizia lowasa ili kuficha siri kali.NILIANDIKA MSTARI HUU BAADA YA KUFANYA UCHUNGUZI NA KUJIRIDHISHA KUWA MHESHIMIWA NI KIONGOZI BORA SANA NA HASA KWA UAMUZI WAKE WA KUJIUZULU BILA SHINIKIZO KUBWA NA WAKATI KWA NAFASI ALIYOKUWA NAYO YA UWAZIRI MKUU ALIKUWA NA UWEZO WA KUGOMA KUJIUZULU NA HASA KWA KUWA HAKUWA FISADI KAMA ILIVYOSEMWA.

MWEZI WA TATU MWISHONI MWAKA HUU NILITOA WIMBO UNAOKWENDA KWA JINA LA KARIBU DAR AMBAKO NILISEMA dar es salam ingekuwa nchi Rais angekuwa Lowasa huku watu washashtukia kuna mchezo kwenye siasa HAPA NILIKUWA NAMAANISHA KUWA WATU WENGI WANAOISHI DAR WANAWAHI KUJUA MAMBO YA WANASIASA KWA KUWA WANASIASA WANAISHI HUKU LAKINI PIA WATAFITI WENGI WA MAMBO YA KISIASA WANAISHI HUKU KWA HIYO NI RAHISI ZAIDI KUUJUA UKWELI MAPEMA.

NAAMINI KUONDOKA KWA LOWASA KWENYE UWAZIRI MKUU KUMEZOROTESHA MAENDELEO YA TAIFA KWA KIASI FLANI

NDUGU ZANGU WATANZANIA NI WAZI KUWA LOWASA NI JEMBE TENA JEMBE LA KAZI KUMBUKENI BILA LOWASA KUSINGEKUWA NA SHULE ZA KATA TANZANIA,NA ANGEENDELEA KUWEPO MADARAKANI ALIKUWA NA MPANGO WA KUANZA MCHAKATO WA ZAHANATI ZA KATA.IKUMBUKWE PIA LOWASA NDIYE ALIYESIMAMIA UJENZI WA CHUO CHA UDOM TENA KWA PESA ZA KITANZANIA BILA KUOMBAOMBA VIMIKOPO.

MRADI WA MAJI KUTOKA MWANZA KWENDA SHINYANGA NI KAZI YA LOWASA. ZIPO KAZI NYINGI AMBAZO NIKIZITAJA ZOTE NAWEZA KUJAZA UKURASA.NACHOJARIBU KUSEMA HAPA NI KWA KUWA MIMI NI MSANII NA NI KIOO CHA JAMII NINGEOMBA WEWE MWANAJAMII CHUKUA HATUA YA KUFANYA UCHUNGUZI BINAFSI KUHUSU LOWASA.BILA KUFUATA MKUMBO WA KISIASA NAAMINI UTAKUBALIANA NA MIMI KUWA LOWASA NI JEMBE.

MIMI HUWA NAPENDA KUSOMA VITABU VYA WANAHARAKATI NA KUNA KITABU KIMOJA NILIKIPITIA CHA MWANAHARAKATI KUTOKA ITALY AITWAE NICCOLO MACHIAVELLI AMBAYE ALIZALIWA MWAKA 1469 NA KUFARIKI 1527. KATIKA ENZI ZA UHAI WAKE ALIWAHI KUANDIKA VITABU KADHAA LAKINI KATI YA VITABU HIVYO KITABU KIITWACHO THE PRINCE NDICHO KILIMPA HESHIMA KUBWA SANA KWA KUWA ALIIKOSOA SERIKALI YA KIFALME YA KIPINDI HICHO KITU AMBACHO HAKIKUWA RAHISI KWA MTU KUFANYA HASA IKIKUMBUKWA KUWA ENZI ZA UFALME ZILIKUWA ENZI ZA UBABE. KATIKA MANENO KUTOKA KWENYE KITABU HICHO AMBAYO NINGE PENDA KUKUSHIRIKISHA WEWE NDUGU YANGU MTANZANIA NI MANENO YAFUATAYO MACHIAVELLI ALIANDIKA HIVI. kuna kipindi ambacho mataifa yanapita katika vipindi vigumu. na kwa kipindi hicho kigumu mataifa hayo yatahitaji sana kupata kiongozi mwenye kuweza kuchukua maamuzi magumu,na ambaye hatakuwa chini ya sauti ya mtu mwingine, na ambaye ataweza kuyatekeleza maamuzi magumu kwa haraka hata kama ni kwa kuwaumiza wachache ili wengi wawe huru.atakayekuwa tayari kutekeleza jambo baya ili likapita na kusahaulika na atakayetekeleza mambo mazuri kwa muda mrefu na yakaendlea kukumbukwa.kiongozi huyo atatakiwa kuchagua kuogopwa ama kupendwa lakini ni bora akachagua kuogopwa lakini akitenda haki kwa wananchi husika.HAYO NI BAADHI YA MANENO ALIYOANDIKA MACHIAVELLI KWENYE THE PRINCE KITABU AMBACHO KILIMPELEKEA KUITWA NA MFALME NA KUPEWA NAFASI YA JUU YA UONGOZI KATIKA SERIKALI HIYO YA KIFALME.

KWA MAONI YANGU NADHANI TAIFA LETU LIMEPITIA VIPINDI VIGUMU KADHAA NA KWA MANENO YA BWANA MACHIAVELLI NADHANI KIONGOZI ANAYEFAA AMBAYE ANAWEZA AKACHUKUA MAAMUZI MAGUMU NA AMBAYE HAWEZI KUWA CHINI YA SAUTI YA MTU MWINGINE NI MHESHIMIWA EDWARD NGOYAI LOWASA.

tafakari chukua hatua


0 comments:

Uliwahi kuwaza kupima malaria kutafikia kutumia application ya simu kama hivi?

mini-IMAGINE2-e1374124657569

Sanyansi na teknolojia ndio vitu vinavyo run dunia kwa sasa, unaambiwa kutokana na ugunduzi ambao Microsoft wenyewe wameutambua na kuwapa zawadi ya dola za Kimarekani elfu kumi na mbili vijana waliofanikisha ugunduzi huo, hivi sasa inawezekana kupima malaria bila hata kutoa damu lakini hapohapo doctor wako akatumiwa taarifa za vipimo kwa njia ya electronic.
Kwenye mashindano ya  Microsoft Imagine Cup kwa ajili ya vijana, vijana wanne kutoka Uganda wameweza kujishindia kiasi cha zaidi ya millioni 19 za kitanzania kwa kutengeneza Windows Application ambayo inafanya kazi na kifaa kingine kidogo cha nje ambacho mgonjwa anaweka kidole kama inavyoonekana kwenye picha ili application itoe majibu ya hali ya malaria mwilini.
Application hiyo waliyoipa jina la Matibabu kwa sasa inafanya kazi  na windows phone lakini ili uweze kupima malaria unahitaji hiki kifaa cha nje.
safe_image

0 comments:

Alcantara;man united hawakunitaka...!!!

Kiungo wa Bayern Munich Thiago Alcantara amesema kwamba ssio kweli kwamba alikataa kujiunga na Manchester United kama ilivyokuwa ikiripotiwa bali klabu hiyo ya England haikuwahi kumtaka hata siku moja.

Thiago alihusishwa sana kutakiwa na United kwenye dirisha hili la usajili kabla ya kuamua kujiunga na mabingwa wa ulaya mapema mwezi huu. 


Jana jumatano, baba yake Thiago, Mazinho aliiambia La Xarxa kwamba mtoto wake alikuwa anakaribia kwenda Old Trafford, lakini Thiago mwenyewe leo amekanusha taarifa hizo.

"Ukweli ni kwamba hakuna muda wowote ambao Manchester United walikuja kuongea na sisi. Mambo yote yalikuwa yakiandikwa na vyombo vya habari, ulikuwa niuongo dhahiri," aliiambia radio RAC1.

Akizungumzia uamuzi wake wa kuondoka Barcelona, alisema: "Sio sahihi kusema kwamba sikuwa mvumilivu. Klabu ilielewa hali yangu. Niliwasubiria wao, lakini hawakuwa wanawasiliana nami. Sikuhisi kwamba nina thamani kwao. 

"Nilitaka kushindana. Klabu ilitambua kwamba nataka kuondoka na hawakufanya lolote kubadilisha hilo.
"Kila mtu anaangalia maslahi yake, nilitaka kuona nathaminiwa na nilitaka kushindana hivyo niliamua kuondoka na kujiunga na Bayern.
"Niliwasubiri sana kipindi chote cha kiangazi na mwishowe nikaamua kufanya uamuzi mgumu.
"Anachokitaka kila mwanasoka ni kucheza soka na nilitaka kucheza, wao [Barcelona] hawakufanya chochote kunihakikishia hilo, hivyo ndio maana sasa nipo hapa."

0 comments:

KIUNGO WA AZAM HUMPHREY MIENO ATAJWA KWENDA KUZIBA NAFASI YA WANYAMA CELTIC


Victor Wanyama ameondoka Celtic Football Club na kujiunga na klabu inayoshiriki kwenye ligi kuu ya England - Southampto baada ya kukamilisha uhamisho wa wa £12.5million. Sasa ikiwa ni wiki kadhaa tangu kiungo huyo wa Kenya kuondoka, kocha wa Celtic Neil Lennon, amesema Wanyama alikuwa ndio kiungo wake bora wa ushambuliaji kwenye timu yake na sasa wanahitaji mbadala wake.
Kutokana na hilo sasa zimeibuka taarifa kwamba kocha huyo ambaye ni nahodha wa zamani wa Celtic anamuwania kiungo mwingine kutoka Kenya Humphrey Mieno. Mieno ambaye kwa sasa ni mchezaji wa Azam FC  inayoshiriki kwenye ligi kuu ya Tanzania.
Celtic, itabidi ifanye haraka kumsaini mchezaji huyo wa Azam FC kwa kuwa kuna vilabu vingi barani Afrika kama miamba ya soka ya Tunisia Esperance na Club Africain zinamuwania kwa nguvu mchezaji huyo ambaye alihamia Azam akitokea Sofapaka ya Kenya.
Mpaka sasa sio Celtic wala Azam FC ambazo zimethibitisha kuhusu taarifa hizi.

0 comments:

HIKI NDIO KINYWAJI RASMI CHA FC BARCELONA NDANI YA BARA LA AFRIKA - WAMPA RAISI KIKWETE JEZI YA NEYMAR

Kushilla Thomas, Mkurugenzi wa Masoko wa Tanzania Breweries Limited (TBL) nje ya ofisi za FC Barcelona huko Catalonia Hispania leo hii baada ya kutangazwa kwa udhamini wa Castle Lager kwa Barcelona.
Bia ya Castle Lager imeingia makubaliano ya kuidhamini moja ya klabu maarufu zaidi duniani ya FC Barcelona ya Hispania kwa kipindi cha miaka mitatu udhamini utakaokifanya kinywaji hicho kuwa bia rasmi ya FC Barcelona barani Afrika. 
Klabu ya FC Barcelona pia imempa zawadi ya Raisi Jakaya Kikwete kwa kutambua mchango wake kwenye maendeleo ya soka nchini
Ushirikiano huu, uliyosainiwa kwenye uwanja wa klabu Camp Nou, unaifanya CASTLE Lager kuwa bia rasmi itakayotumika kwa shughuli yoyote ambayo Barcelona itashiriki kwenye bara la Afrika na pia itafungua milango kwa mashabiki wa Barcelona Afrika kuwa karibu na wachezaji wa Barcelona, vifaa, na kumbukumbu. Pia kupata nafasi ya kusafiri kwenda Hispania kushuhudia kwa karibu timu ya Barcelona. 
Mkataba huu utakuwa maalum kwa ajili ya CASTLE Lager kwenye nchi nyingi za Afrika isipokuwa kwa baadhi ya nchi chache zilizochaguliwa ambapo itatumika Castle Milk Stout.
Hii ni mara ya kwanza kwa timu ya FC Barcelona kusaini mkataba wa udhamini na kampuni ya bara la Afrika. Kushirikiana na bia bingwa Afrika litaongeza kwa haraka umaarufu wa timu ya FC Barcelona ndani ya bara la Afrika na kufungua milango kwa mashabiki wa klabu hii kupata bidhaa mbalimbali za Barcelona na nafasi za kushinda safari ya kwenda Barcelona kuitembelea klabu hiyo. 
Wawakilishi wa SABMiller kutoka nchi mbalimbali barani Afrika wakiwa nje ya ofisi ya FC Barcelona uko Catalonia Hispania leo hii
Tumefurahi sana kuingia katika ushirikiano na Castle Lager na Castle Milk Stout, chapa zinayofahamika dunia nzima . Tunafanana na Castle kwa kuwa sote tuna historia ya zaidi ya miaka 100 na utamaduni uliotukuka. Na sote tuna mapenzi na mpira wa miguu pamoja na mashabiki wake katika soko muhimu kama Afrika,” alisema Javier Faus, Makamu wa Rais wa FC Barcelona anayeshughulikia masuala ya uchumi.
Mkurugenzi wa Masoko wa TBL, Kushilla Thomas akimkabidhi zawadi ya asili kutoka Tanzania Bw. Javier Faus, Makamu wa Rais wa FC Barcelona anayeshughulikia uchumi huko Catalonia Hispania leo hii baada ya kutangazwa kwa udhamini wa Castle Lager kwa Barcelona.
 “Uamuzi wa Barcelona kuingia ushirika na na bia inayoongoza barani Afrika kutaongeza umaarufu wa bia hiyo kwenye bara hili na kuwawezesha wachezaji wa timu hiyo kufika maeneo amabyo hawajawahi kufika barani Afrika,” alisema David  Carruthers Mkurugenzi wa Masoko wa SabMiller Afrika (kampuni mama ya TBL).
CASTLE Lager si bidhaa mpya kwenye udhamini wa mpira wa miguu na vyama, ina miaka mingi ya kujihusisha katika soka barani Afrika kwa kipindi cha miaka 85 kupitia ligi mbalimbali za nchi tofauti kama vile Zimbabwe, Swaziland, Botswana, Lesotho na pia mashindano ya kanda kama COSAFA Kusini mwa Afrika na CECAFA Afrika Mashariki.
Kutokana na soka la Ulaya kupata umaarufu mkubwa na mashabiki wengi barani Afrika, Castle Lager imekuwa ikidhamini urushaji wa matangazo ya ligi hizo kwenye televisheni barani Afrikana kuwapa mashabiki fursa ya kufatilia kila kinachoendelea kwenye ligi hizo maarufu duniani ambazo ni Ligi Kuu ya Ulaya, Ligi Kuu ya Uingereza na La Liga ya Kihispania.
Kufuatia udhamini huu, wanywaji wa Castle Lager na Castle Milk Stout pamoja na mashabiki wa Barcelona barani Afrika sasa watarajie mambo mengi ya kusisimua katika ulimwengu wa soka.

0 comments:

KOCHA MPYA WA BARCELONA AWAAMBIA MAN UNITED - 'NITAIKATAA OFA MPYA YA UNITED KUMNUNUA FABREGAS"

Gerardo Martino amemwambia David Moyes kwamba Cesc Fabregas hauzwi baada ya kutambulishwa rasmi kuwa kocha mpya wa klabu ya FC Barcelona kwa mkataba wa miaka miwili.

Kocha huyo wa zamani wa Newell's Old Boys amerithi mikoba ya Tito Vilanova, ambaye alilazimika kujiuzulu kutokana matatizo yake ya kiafya.

Akiongea kwenye mkutano wa waandishi wa habari leo Ijumaa, Martino alisema: 'Man United inamtaka Cesc? Kama klabu ilikataa ofa mbili za kwanza, mie nitaikataa ya tatu. Cesc atabaki hapa.'

Makamu wa Raisi wa Barca Josep Maria Bartomeu amethibitisha maneno ya Martino, akiongeza: 'Ni kawaida United kuvutiwa na mchezaji, lakini tunamtegemea Cesc na hatutomuuza, haijalishi watatoa ofa ya kiasi gani.'

0 comments:

AZAM TV YALIPA BILLIONI 6.5 ILI KUONYESHA MECHI ZA LIGI KUU YA TANZANIA BARA


 
Badhi ya viongozi wa TFF wakisaini mikataba na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Azam, Said Mohammed (wa kwanza kulia) leo kwenye Ofisi za TFF zilizopo Karume jijini Dar es Salaam.
Televisheni ya Azam inayojulikana kama Azam TV imeingia mkataba wa miaka mitatu wa kuonesha michuano ya Ligi Kuu Tanzania Bara na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ambapo mkataba huo umetajwa kuwa na thamani ya Tsh bilioni 6.5
Aidha Televisheni hiyo itakuwa na majukumu ya kuonesha mechi za moja kwa moja (LIVE) zisizopungua 60 za Ligi hiyo huku nyingine 180 zikiwa zimerekodiwa.

SOURCE: GLOBAL PUBLISHER

0 comments:

HARUNA CHANONGO - SINA AKAUNTI FACEBOOK - ANAYETUMIA JINA LANGU KWENYE MTANDAO HUO NI FEKI

Winga wa timu ya taifa ya Tanzania anayekipiga klabu ya Simba Haruna Chanongo amasema amesikitshwa mno na kitendo cha mtu asiyefahamika kutumia jina lake na picha kwenye mtandao wa Facebook.

Akizungumza na mtandao huu kutoka Kampala alipo na timu ya taifa ya Tanzania inayojiandaa kucheza mechi ya pili kuwania nafasi ya kucheza kombe la CHAN, amesema yeye binafsi hana akaunti kwenye mtandao wa kijamii wa FACEBOOK lakini anashangaa amekuwa akipokea malalamiko kutoka kwa watu wa karibu kuhusu suala la akaunti hiyo.

"Kiukweli mie sina akaunti Facebook, sasa nashangaa muda mwingine napata malalamiko kutoka kwa watu wangu wa karibu na hata mashabiki kuhusu mambo ya ajabu huyo aliyofungua hiyo akaunti anayafanya. Ninachotaka kuweka wazi mie sina akaunti Facebook hivyo watu wote wafahamu kuhusu hilo," alimaliza Chanango amepa kwamba leo akipata nafasi atajitahidi kwa hali na mali kuiwezesha Tanzania kufuzu.


FAKE ACCOUNT

0 comments:

MAKALA: WAYNE ROONEY HANA WA KUMLAUMU KWA YANAYOMTOKEA - ANAONJA UTAMU WA DAWA ZAKE MWENYEWE

Wayne Rooney's testy relationship with now-retired manager Sir Alex Ferguson contributed to Rooney wanting to leave Manchester United in 2010.

Umetaarisha kitanda chako, sasa inabidi ukilalie. Kinachoenda huwa kina tabia ya kurudi. Unaishi kwa upanga utakufa kwa upanga. Unavuna ulichopanda. Vyovyote unavyoweza kuyasema maneno haya, hili suala la Wayne Rooney 'kuwa na hasira na kuachnganyikiwa' kuhusu nafasi yake ndani ya Manchester United -- ni jambo ambalo amejitakia mwenyewe.

Baadhi ya wachambuzi wa soka wamekuwa wakisema kwamba lilianza katika wiki za mwisho za utawala wa Sir Alex Ferguson kama kocha wa United, alipomuacha Rooney nje kwenye mechi za Champions League dhidi ya Real Madrid, na baada ya wiki kadhaa mchezaji akaomba kuuzwa kwa mujibu wa Fergie. Lakini hatua hii ni mojawapo baada ya sakata la Rooney kuomba kuondoka mwaka 2010 akitishia kwenda Manchester City ---jambo lilopelekea matusi mengi kuelekezwa kwake wakati akiwa bado ameomba kuondoka -- lakini hatimaye akaamua kubaki baada ya kupewa mkataba mpya mnono wa miaka mitano. '

Tangazo la Rooney mwishoni mwa mwaka 2010 halikutokea ghafla tu: yeye na Ferguson walianza kuzozana kuhusu majeruhi ya enka. Baada ya muda kidogo kabla ya mzozo huo wa majeruhi ya Rooney, ikatoka taarifa kwamba mshambuliaji huyo ameomba kuhama, alitoa taarifa rasmi akisema kwamba alikutana na klabu kuhusu mkataba wake mpya, na alitaka uhakika kuhusu uwezo wa klabu kuvutia wachezaji wakubwa duniani - jambo ambalo aliliona ni gumu kwa klabu kulifanikisha. 
'UNITED HAINA UWEZO WA KUFIKIA MATAMANIO YANGU',  vichwa vya habari vya magazeti na mitandao ya viliandika siku iliyofuata. City walisema walikuwa wanafuatilia kwa ukaribu sakata hilo la Rooney na United; kundi la mashabiki wenye hasira lilikusanyika nje ya nyumba ya Rooney kumtolea vitisho vya kumuua endapo angahamia upande wa pili wa mji wa Manchester.

Hiyo ilikuwa kati kati ya wiki. Ijumaa iliyofuatia Rooney akasaini mkataba mpya, akitoa sababu kwamba United walimhakikishia kwamba wana uwezo wa kuendelea kushindana kwenye hatua ya juu kabisa. "Siku zote wasiwasi wangu ulikuwa ni kuhusu siku za mbeleni. Katika siku kadhaa zilizopita, nimeongea na kocha na wamiliki ..... ninasaini mkataba mpya nikiwa naamini kabisa kwamba utawala, benchi la ufundi na bodi pamoja na wamiliki watahakikisha United inaendelea kuimarisha historia yao nzuri ya ushindi."

Pia wakawa wameongeza mara mbili mshahara wake. Toka wakati huo Ferguson hakuwa na mahusiano ya karibu mno na mchezaji husika; alikuwa kama mzee ambaye amelipwa mafao yake ya uzeeni, halafu akatokea kijana ambaye alimuonyesha paa lake limechakaa likiwa kwenye hali mbaya, lakini akamwambia angemsaidia kulitengeneza kwa kiasi cha fedha chote alicholipwa kwenye mafao yake.

Labda Ferguson aliamua tu kujishusha na kuweka mambo sawa: Rooney alikuwa kwenye kiwango bora kabisa msimu wa 2009-10, akifunga mabao 34 na kutajwa kuwa mchezaji bora wa mwaka wa wachezaji wa EPL.  Pamoja na tabia yake ya kuweka mbele klabu ya mtu yoyote, Ferguson amekuwa akiwapa nafasi kubwa wachezaji, pale anapohisi mchango wao uwanjani una faida kwa timu. Hali hiyo ilibidi iendelee baada ya Fergie kukubali ushauri wa Rooney kwamba inabidi kuhakikisha klabu inasajili wachezaji wakubwa wataohakikisha timu inaendelea kuwa juu.

Msimu mmoja baadae baada ya Manchester City kushinda ubingwa mbele ya United kwa tofauti ya mabao msimu wa 2011-12, Ferguson akampa Rooney alichokuwa anakitaka - uhakika wa kufanya vizuri kwa kumsaini Robin van Persie, mmiliki wa kiatu cha dhahabu cha EPL na mchezaji bora wa ligi msimu huo, akitokea Arsenal. Aina ya mshambuliaji ambaye Rooney alikuwa anamtaka ndani yake. Van Persiealifunga mabao manne katika mechi zake tatu za kwanza za United, na kutoa ishara kwamba makubwa zaidi yanakuja. Mabao yake, Ferguson alisema ndio yaliyorudisha kombe Old Trafford.

Usajili wa Shinji Kagawa nao ukaongeza uhakika anaoutaka Rooney. Mjapan huyu alipokuwa akicheza, alikuwa akichezeshwa alikuwa akionyesha kwamba anaweza kucheza namba 10 - jukumu ambalo Rooney alikuwa amepewa baada ya ujio wa Van Persie. 

Rooney huwa anaamika hakuwa amependa kucheza kwenye kiungo aliporudishwa; United wanaona wana watu au mtu wa kuziba nafasi yake katika namna ambayo hawakuwa na uwezo huo mwaka 2010 alipoomba kuondoka. Ikiwa United wataweza kumsajli  Cesc Fabregas kutoka Barcelona, hali ya ulazima wa kuwa na Rooney itazidi kupungua. 

Wakiwa tayari wameshakataa ofa ya $30.5 million kutoka kwa Chelsea, United wanasisitiza Rooney hauzwi. Huku Moyes akisema kwamba atamhitaji Rooney endapo Van Persie atakuwa majeruhi kwa maana ya nafasi ya ushambuliaji. Kwenye kiungo akiwa anataka kuongeza watu wengine wawili tena akitaka kwa kuwanunua kwa bei mbaya ina maana wanakuja kuingia moja kwa moja kwenye kikosi cha kwanza.

Sasa Je Rooney ana hasira na amechanganyikiwa kwa kugundua kwamba hana namba ya kdumu kama zamani au kauli za kocha wake mpya kwamba atamhitaji kama spea tairi kwa RobinVan Persie?
  
Je Rooney ana hasira na kuchanganyikiwa kwa sababu hizo? Au ameshikwa nayvu za mtego alioutengeneza mwenyewe?

Wayne Rooney hana wa kumlaumu kuhusu hili zaidi yake ya mwenyewe.

0 comments:

beyonce avarishwa nguo na mbunifu wa bongo..

Mbunifu wa mavazi Mtanzania Christine Muhando amesema kapata zaidi ya oda 100 baada ya Beyonce kuvaa nguo yake.
 

0 comments:

mWanafunzi afariki baada yakuzidiwa mazoezi...

Mwanafunzi anaedaiwa kufariki Tabora baada ya kuzidiwa na mazoezi ya Jeshi, Halima Kitangilwa (20) amezikwa leo Dar.

Baba yake amesema amedanganywa kuhusu chanzo cha kifo lakini ndugu zake waliokuwepo jeshini wamemwambia ukweli, analaumu pia hajapewa ripoti ya uchunguzi wa mwili.

Naendelea kumtafuta msemaji wa JKT kujua upande wao unasemaje.@millad ayo

0 comments:

dj haleed aomba ndoa na nikki minaj kwenye MTV liveee...



MTV received an exclusive video proposal from DJ Khaled. The 37-year-old proposed to Nicki Minaj and offered her a 10 karat engagement ring. Minaj was not in the studio and has not responded to the proposal. Although they share a music label, they have not been romantically linked in the past.
In the video, DJ Khaled states he is in love with Nicki Minaj and wants to marry her. He mentions that he wanted to propose to Nicki last year but decided to wait and buy a stunning engagement ring. The large 10 karat diamond ring is estimated to be worth $500,000. MTV claims he purchased the ring from Rafaello & Co.
He promises to take care of Nicki and respect her, but he also wants to give her time to respond to his proposal. He holds out the engagement ring inside its black leather box to the camera and asks Nicki to marry him. The video ends with the words “Your move, Nicki.” Minaj has not publicly responded to DJ Khaled or MTV. Her representatives are also staying silent, and Khaled’s reps are not confirming if this was just a publicity stunt.

0 comments:

photo:tazama;umepata kuona mwezin kukoje?

0 comments:

ROONEY ANAWEZA KUFIKIRIA KUJIUNGA NA ASERNAL, LAKINI KAMA DILI LA CHELSEA LITAGONGA MWAMBA!!

Mshambuliaji wa Manchester ambaye kwa sasa hajatulia klabuni hapo, baba wa watoto wawili, Wayne Mark Roonye huenda akafirikiria kwenda washika bunduki wa kaskazini mwa London, klabu ya Asernal endao ndoto yake ya kufanya kazi na kocha wa Chelsea, Jose Mourinho haitatimia.
Manchester United wanakataa kumuuza Rooney kwa wapinzani wao wakubwa wa kuwania ubingwa msimu ujao, lakini bado nyota huyo anataka kuondoka Old Trafford.
Ingawa Chelsea ni chuguo la kwanza kwa Rooney, mshambuliaji huyo raia wa England anaweza kwenda Arsenal endapo David Moyes na bodi ya timu hiyo watakataa ofa ya pili ya Jose Mourinho.
Departing? Wayne Rooney is a target for both Arsenal and ChelseaAnaondoka? Wayne Rooney anawindwa na klabu za Arsenal na Chelsea
Arsenal walianza harakati za kumtaka Roonye ambaye atafikisha miaka 28 mwaka huu wakati ule amepigwa benchi na Sir Alex Ferguson katika mechi muhimu ya ligi ya mabingwa barani Ulaya dhidi ya Real Madrid mwezi machi mwaka huu.
Arsenal wameonesha kuwa wanaweza kumlipa Rooney mshahara mzuri. Kwa sasa nyota huyo analipwa pauni milioni mbili  na elfu arobaini kwa wiki na amebakisha miaka miwili katika mkataba wake, lakini The Gunners watavunja rekodi ya klabu kwa kumlipa pauni lakini mbili kwa wiki na mkataba wa miaka mitano.
Lakini Chelsea bado wanaongoza mbio za kumsainisha Roonye baada ya kutuma ofa ya pauni milioni 23, na kuongeza2.5 wiki iliyopita.
Baada ya kupata majeruhi ya nyama za paja katika ziara yao ya maandalizi ya msimu mpya wa ligi kuu, Rooney anaendelea na mazoezi mepesi  katika uwanja wao wa Carrington, huku akiwa na matumani kuwa klabu hizo mbili zitakubaliana juu ya yeye kuihama United.
Mama watoto wa Rooney,  Coleen anaonekana kukubaliana na mume wake na ameweka wazi kuwa anapenda kuishi jijini London na watoto wao.
Jose Mourinho
Arsene Wenger
 Ushindani: Jose Mourinho na  Arsene Wenger wote wanamhitaji Rooney kutoka United
Under pressure? David Moyes could be on the verge of losing one of his best playersAna presha kubwa? David Moyes anaweza kumpoteza moja kati ya majembe ya United
Rooney alizungumza kwa njia ya simu na kocha  Moyes pamoja na mkurugenzi mkuu  Ed Woodward baada ya kutokea tofauti kati yao juu ya umuhimu wake klabuni hapo.
Chelsea wanajiandaa kuongeza mzigo ili kumnasa Rooney, na taarifa zilizopatikana ni kuwa wanaandaa pauni milioni 30.
Kama United watakaa kumuuza Chelsea, basi itakuwa habari njema kwa Asernal kabla ya kumalizika kwa muda wa dirisha la usajili.

0 comments:

Tozo za simu sasa kuangaliwa upya

Dar es Salaam. Serikali imekubali kupitia mawazo na maoni yaliyotolewa na Umoja wa Wamiliki wa Kampuni za Simu Nchini (MOAT), kuhusu kufutwa kwa tozo ya kodi ya laini za simu ‘Simcard tax’ ya Sh1000 kutokana na kulalamikiwa na wadau wa sekta ya mawasiliano.
Hali hiyo inatokana na kauli za viongozi wa Serikali, wabunge na wananchi wanaopinga tozo hiyo kwa kile wanachokieleza kitaongeza mzigo wa ugumu wa maisha kwa mtumiaji hususan wa kipato cha chini.
Waziri wa Fedha, Dk William Mgimwa akizungumza na wandishi wa habari jana alisema, wamekutana na MOAT na kupokea mapendekezo yao na sasa wanayafanyika kazi.
“Tumeendelea kusikia malalamiko kutoka pande mbalimbali na juzi, tulikutana na MOAT na tumejadiliana na wametoa mapendekezo mazuri tu kipi kifanyike ili tupunguze makali ya kodi hii hususan kwa wananchi wa hali ya chini,” alisema Dk Mgimwa na kuongeza:
“Katika suala hili, jazba zisiwepo kwani ni suala la kisheria kutokana na kupitishwa bungeni hivyo ili kuondolewa ni lazima kufuata mkondo na tunatizama mapendekezo ya jinsi ya kulishughulikia.”
Dk Mgimwa aliendelea kusema “Hakuna mtu anayelenga kumkamua mwananchi,lakini hili lilitokana na mapendekezo 67 yaliyotolewa na Kamati ya Bajeti kuwa chanzo cha mapato kinachotekelezeka lakini kama inaonekana kuwa kikwazo tutangalia jinsi ya kukabiliana nalo.”
Waziri huyo alisema lengo la tozo hiyo ilikuwa kupata fedha zitakazoelekezwa katika miradi ya maji, barabara na umeme hususani vijijini kunakokabiliwa na changamoto mbalimbali muhimu za maendeleo.
Alisema mpaka sasa hakuna mtumiaji wa huduma hiyo ambaye ameanza kukatwa tozo hiyo kutokana na mchakato huo kuwa bado unaendelea katika utekelezaji wake.
Naye Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa alisema, Serikali itahakikisha mwananchi hapati mzigo usiokuwa na sababu.
“Serikali ni sikivu na inaNacho chama tawala, CCM,Chadema walikaririwa na vyombo vya habari wakiitaka Serikali kuangalia vyanzo vingine vya mapato badala ya tozo hiyowasikiliza wananchi wake hivyo kupitia mawazo na mapendekezo mbalimbali yaliyotolewa yanafanyiwa kazi ili kutokuathiri pande zozote,” alisema Profesa Mbarawa.
Profesa Mbarawa alisema, uwekezaji hususani vijini umekuwa ukikabiliwa na changamoto za miundombinu ya barabara, umeme na maji vitu ambavyo vikiboreshwa vitawavutia wawekezaji wengi.
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba Juzi alisema, wizara hiyo ilipinga tangu awali mpango huo kabla ya kupitishwa na kuwa sheria na kwamba anaamini itaondolewa.

0 comments:

Zanzibar iwe mkoa wa Tanzania

Sumbawanga. BAADHI ya wajumbe wa Baraza la Katiba la Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa, wametaka katika katiba ijayo kuwe na muundo wa Serikali moja, huku Zanzibar ikiwa ni moja ya mikoa ya nchi ya Tanzania na iwapo Wazanzibari watakataa, waruhusiwe kujitenga.
Mmoja wa wajumbe wa baraza hilo la Katiba Wilaya ya Kalambo, Afred Ntinda mkazi wa kata ya Mwazye kijiji cha Mpenje alisema hayo jana wakati akichangia maoni katika kikao cha baraza hilo kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya wilaya mjini hapa.
Mpenje alisema kuwa mfumo wa sasa wa Serikali mbili una kasoro nyingi na umeshindwa kutatua kero za Muungano hivyo hautakiwi kuendelea kuwepo wakati ule wa Serikali tatu hawezi kulinda muungano huo kwa kuwa Serikali hizo zinaweza kuongozwa na marais kutoka vyama tofauti vya siasa na wenye mitizamo isiyolingana hivyo kuna hatari ya muungano kuvunjika.
“Sisi huku bara kuwa na Serikali moja si tatizo wengi wataridhia, nafikiri kuna tatizo katika upokeaji wa maoni kwa wenzetu wa Zanzibar.

0 comments:

Brazil yajiandaa.....!!!!


Nchi yajawa na msisimko

 Siku zinaendelea kuhesabiwa tayari kwa kombe la dunia. Wakati timu ya taifa ya Brazil ikiendelea kujiimarisha, mashabiki tayari wamejawa na msisimko. Mashabiki wa kabumbu wa Brazil wanaonekana kuwa machachari sana kote ulimwenguni, na hata katika picha hii, filimbi zao ni kama zina kelele nyingi kuliko vigelegele vyao.

0 comments:

"BIKIRA MARIA AONEKANA KANISANI.

Bikira Maria Picha juu ni ya Kanisa la Kikatoliki la Saint Benedict, lililopo Ubiaja, Esan Kusini Mashariki ya Jimbo la Edo nchini Nigeria.


Waumini wa Kanisa hilo wanasema kwamba waliiona kitu kinachofanana na Bikira Maria kwenye ukuta wa Kanisa hilo mnamo siku ya Jumapili July 21.

 Waumini hao walifanikiwa kuchukua picha....
Je unaiona? Je inahitaji maelezo ya ziada juu ya hili?
Angalia na picha hapo juu...?

0 comments:

Mark Zuckerberg alishawahi kuhisi 50 Cent amefanya kazi kwake (facebook)


50 Cents hajawahi kumaliza high school, lakini alishawahi kuaminiwa kuwa "mkuu wa maendeleo ya biashara  na mauzo" kupitia facebook 2005.
Wakati nafasi ya  mwanzilishi mwenza wa Facebook, Saverin Eduardo (mkuu wa maendeleo ya biashara  na mauzo) kuchukuliwa na Kevin Colleran, Zuckerberg alimchanganya kijana huyo na mega superstar 50 Cent kutokana na picha ya profile yake inayomuonyesha akiwa na 5o Cent.

Hivi ndivyo jinsi ilivyokuwa siku ya kwanza walipokutana Zuckerberg na Colleran uso kwa uso..
Zuckerberg alipanga kukutana na Colleran mbele ya Virgin  Megastore iliyopo New York Union Square, Colleran alifika akiwa amechelewa na hivyo kuelekea moja kwa  moja alipo Zuckerberg huku akipokea simu kutoka kwa huyo huyo Zukerberg akimuuliza "Uko wapi", Colleran akamjibu nimpo mbele yako. Zuck alimuangalia kwa mshangao sana, alidhani muuza matangazo ya facebook ni yule jamaa aliekuwa akionekana  mweusi na tafu sana kwenye profile picture (50 Cents)
Rais wa Facebook na mwanzilishi wa Napster, Sean Parker alimwambia Colleran kuwa mkutano na Zuckerberg ulikuwa wired sana sababu "sisi tulidhani ungekuwa African-American."
Wakati wa mkutano wao, 50 Cent alikuwa tayari kashauzwa rekodi zaidi ya milioni 8 na album yake ya kwanza Get Rich Or Die Trying, na moja ya single zilizofanikiwa sana kwenye radio kwa muda wote  "In Da Club" na alikuwa kashasainiwa Dr Dre na Eminem.

0 comments: